Yawe alituma manabii na waonaji kuionya inchi ya Israeli na ya Yuda akisema: “Mwache njia zenu mbaya mutii amri zangu na masharti yangu kufuatana na sheria nilizowapa babu zenu, na ambazo niliwapa ninyi kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
Walikataa kutii masharti yake; hawakushika agano alilofanya na babu zao, walizarau maonyo yake, waliabudu sanamu zisizokuwa na maana hata wao wenyewe hawakukuwa na maana tena, walifuata desturi za mataifa yaliyowazunguka: walizarau amri za Yawe; wala hawakuzishika.
Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–
Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.
Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.
“Mungu wa miungu ndiye Yawe! Mungu wa miungu ndiye Yawe! Yeye anajua kwa nini tumefanya hivyo. Na Waisraeli wote watajua vilevile! Kama huu ni uasi au ni ukosefu wa imani kwa Yawe basi, yeye aache kutuokoa leo.