Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa! –Ni ujumbe wa Yawe.– Wamejaza nyumba zao nzuri na vitu vya wizi na mateso.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 3:10
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha kula hakuacha hata makombo. Kwa hiyo fanaka yake yote haitadumu.


Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate, wala hawajali Yawe.


Tutajitwalia mali zote za bei kali, tutazijaza nyumba zetu vitu tulivyonyanganya.


Mwanamuke mwema anaheshimiwa; wanaume wenye nguvu wanatajirika.


Waovu hawaelewi haki ya sheria, lakini wanaomwogopa Yawe wanaielewa kabisa.


Kisha nikaona mateso yote yanayofanyika chini ya jua. Watu wanaogandamizwa wanalia machozi, lakini hakuna mutu yeyote anayewafariji. Wagandamizaji wao wana nguvu, ndiyo sababu hakuna wa kuwafariji.


Yawe anasema: Watu wangu ni wapumbafu, hawanijui mimi. Wao ni watoto wajinga; hawana ufahamu. Wao wanaelewa vizuri kutenda maovu, lakini hawajui kutenda mema.


Kwa hiyo niliwaza hivi: Watu hawa ni zaifu, hawana akili; hawajui mapenzi ya Yawe, hawajui Sheria ya Mungu wao.


Kila fasi katika inchi watu wanatendeana vibaya na kunyanganya kwa kinguvu. Wanagandamiza wamasikini na wakosefu, na kuwaonea wageni bila kujali.


Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeyaona mambo hayo? Hata hivyo, watu wa Yuda wanaona machukizo hayo kuwa ni kidogo. Wanajaza mateso makali katika inchi na kuzidi kunikasirikisha. Angalia jinsi wananichukiza!


Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele, ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli, uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa, matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza. Wao wanaongozwa na udanganyifu, mwizi anabomoa nyumba; inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Angalisho, enyi munaogeuza sheria kuwa uchungu, na kuona haki kuwa kama takataka!


Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa? Watu wanaweza kulima bahari na ngombe? Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu, na tunda la haki kuwa uchungu.


Ninyi munajaribu kuifukuza ile siku mbaya. Lakini munaukaribisha utawala wa mateso.


Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake: Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo; tena ninachukia nyumba zao nzuri sana. –Ni ujumbe wa Yawe.– Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.


Nitavumilia maovu yaliyolundikwa ndani ya nyumba yao, mali zilizopatikana kwa udanganyifu, na matumizi ya vipimo vya udanganyifu, jambo ambalo ni chukizo?


Siku hiyo nitawaazibu wote wanaoruka kizingiti cha nyumba kama wapagani, wanaojaza nyumba ya bwana wao vitu vya mateso na udanganyifu.


Watu hawa wanasahau kwa makusudi kwamba tangia zamani Mungu alisema tu, na mbingu na dunia vikakuwa. Dunia iliumbwa toka katika maji na kwa njia ya maji.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ