Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wanagandamiza wazaifu, na kuwabagua wamasikini wasipate haki zao. Mutoto na baba yake wanalala na binti mujakazi mumoja, hivyo wanalichafua jina langu takatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 2:7
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, kwa sababu kwa tendo lako umemuzarau kabisa Yawe, mutoto wako atakufa.”


Hapo, Ahabu akarudi kwake akijaa chuki na huzuni nyingi, kwa sababu Naboti wa Yezereheli alimwambia kwamba hatamupa kile alichorizi kutoka kwa wazee wake. Basi, akalala kwenye kitanda, akaficha uso wake na kukataa chakula.


Si vizuri kumubagua mutu. Watu wanafanya mabaya hata kwa ajili ya mukate.


Ole kwao wanaotunga sheria za uovu, watu wanaopitisha sheria za kugandamiza.


Wanakataa kusambisha wazaifu, wananyanganya watu wangu wamasikini haki yao. Wanateka wajane; wananyanganya wayatima mali yao.


Yawe anawashitaki wazee na wakubwa wa watu wake: Ninyi ndio mulioliharibu shamba la mizabibu; mali wamasikini walizonyanganywa ziko ndani ya nyumba zenu.


Muna haki gani kuwagandamiza watu wangu, na kuwatendea wamasikini vibaya? –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.


Wengine wanafanya machukizo kwa kulala na wake za jirani zao. Wengine wanalala na wake za watoto wao, na wengine wanalala na wadada zao.


Hata walipokuwa kati ya mataifa walilikufuru jina langu takatifu, hata watu wakasema hivi juu yao: Hawa ndio wale watu wa Yawe, lakini wamelazimishwa kuondoka katika inchi yake!


Lakini sitawaazibu wabinti zenu wanapofanya uzinzi, wala bibi-arusi wenu wanapofanya uasherati, maana, wanaume wenyewe ndio wanaofuatana na wazinzi, na kutambikia pamoja nao katika ibada za uzinzi. Watu hawa wenye kukosa akili hakika wataangamia!


Usilale na muke wa mwana wako, huyo ni muke wa mwana wako. Usilale naye.


Usimutoe mutoto wako yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki maana kufanya hivyo utazarau jina langu mimi Mungu wako. Mimi ni Yawe.


Usimuvunjie heshima baba yako kwa kulala na mumoja wa wake zake. Hao ni wamama zako.


Mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na kumutenga na watu wake kwa sababu alimutoa mumoja wa watoto wake sadaka kwa mungu Moleki na hivyo akachafua Pahali pangu Patakatifu na jina langu takatifu.


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.


Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu na ukubwa wa zambi zenu; ninyi munawatesa watu wema, munapokea kituliro na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali.


Musikilize, enyi munaowagandamiza wakosefu na kuwaletea maangamizi wamasikini wa inchi.


Wanatamani mashamba na kuyatwaa; wakitaka nyumba, wananyanganya. Wanawatesa wenye nyumba na jamaa zao, wanawanyanganya watu mali zao.


Munawafukuza wake za watu wangu kutoka nyumba zao nzuri. Mumewaondolea watoto wao utukufu wangu milele.


Wakubwa wake ni simba wanaonguruma, waamuzi wake ni imbwa wa pori wenye njaa magaribi wasioacha chochote mpaka asubui.


Kwa maana kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu yenu, jina la Mungu linatukaniwa katikati ya watu wa mataifa mengine.”


Habari inasikilika fasi zote kwamba kunafanyika uzinzi katikati yenu. Wanaeleza kwamba uzinzi huu ni ubaya mukubwa, usiofanyika hata katikati ya wapagani, kwa maana wanasema kwamba kuna mumoja wenu ambaye amekamata muke wa baba yake kuwa muke wake!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ