Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Yuda, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamezarau sheria zangu, wala hawakufuata masharti yangu. Wamepotoshwa na miungu ileile babu zao waliyoifuata.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 2:4
53 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini hata watu wa Yuda hawakutii amri za Yawe, Mungu wao; lakini walifuata desturi zilizoletwa na watu wa Israeli.


Amazia aliporudi kisha kuwashinda Waedomu, akaleta miungu ya Waedomu akaifanya kuwa miungu yake, akainama uso mpaka chini mbele yao na kuifukizia ubani.


Musikuwe kama babu zenu na wandugu zenu ambao hawakukuwa waaminifu kwa Yawe Mungu wa babu zao, ambaye kama vile munavyoona aliwaazibu vikali.


Tumetenda mabaya mbele yako, hatujashika amri zako, masharti na maagizo yako uliyomwagiza mutumishi wako Musa.


Lakini hawakukuwa waaminifu kwako. Wakakuasi, wakaacha sheria yako na kuwaua manabii waliowaonya kusudi wakurudilie wewe. Wakatenda zambi kubwa mbele yako.


Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!


Hapana! Mawazo yao yameambatana na hicho ambacho ni majivu tu! Mutu huyo amepotoka hata hawezi kujiokoa mwenyewe na kusema: Kweli, hiki ninachokuwa nacho katika mukono wangu ni udanganyifu mutupu!


Nawe utawajibu hivi: Babu zenu waliniacha. Wakafuata miungu mingine, wakaitumikia na kuiabudu. Waliniacha, wala hawakuzitii sheria zangu.


Ninyi mumefanya vibaya zaidi kuliko babu zenu, maana kila mumoja wenu ni mwenye moyo mugumu na mwenye nia mbaya, wala hamunisikilizi.


Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.


Sikiliza, ee dunia! Mimi nitawaletea watu hawa hasara kulingana na nia zao mbaya. Maana hawakuyajali maneno yangu, na mafundisho yangu nayo wameyakataa.


Itaachwa imetandazwa mbele ya jua na mwezi na nyota zote za mbingu, vitu ambavyo walivyopenda na kuvitumikia, na kuviendea kwa kuuliza shauri na kuviabudu. Mifupa hiyo haitakusanywa wala kuzikwa, lakini itabaki kama vile mboleo juu ya udongo.


Wenye hekima kati yenu wanafezeheka, watahangaishwa na kunaswa. Wamelikataa neno la Yawe. Basi ni hekima gani wanayokuwa nayo?


Basi, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitawakulisha watu hawa uchungu na kuwapa maji yenye sumu wakunywe.


Kwa sababu mumewavunja watu wa haki moyo kwa kusema uongo, ijapokuwa mimi sikuwavunja moyo, mukawaimarisha waovu wasiache mienendo yao mibaya na kuokoa maisha yao,


Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.


Nilifanya hivyo kwa sababu waliyakataa maagizo yangu, hawakufuata masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu; maana walijitoa kwa moyo juu ya sanamu za miungu yao.


Niliwaonya wazao wao kule katika jangwa: Musifuate masharti ya wazee wenu, musishike maagizo yao wala musijichafue kwa kuziabudu sanamu za miungu yao.


kwa sababu hawakufuata maagizo yangu, lakini waliyakataa masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu na kuziabudu sanamu za miungu ya wazee wao.


Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mutajichafua kwa kufuata desturi za wazee wenu na kuviabudu vitu vinavyonichukiza?


Manabii wake wanaficha maovu hayo kama mutu anapotia chokaa kwenye ukuta wenye kuharibika. Wanapata maono ya uongo na kutabiri udanganyifu mutupu, wakisema “Bwana wetu Yawe anasema hivi”, wakati mimi mwenyewe sikuwaambia chochote.


Wewe umezarau vyombo vyangu vitakatifu na kuzikufuru Sabato zangu.


Watu wa Efuraimu wanachunga upepo, muchana kutwa wanafukuza upepo wa mashariki. Wanazidisha uongo na mateso, wanafanya mapatano na Asuria na kupeleka mafuta Misri.


Yawe ana mashitaki juu ya Yuda; atawaazibu wazao wa Yakobo kadiri ya makosa yao, na kuwalipa kadiri ya matendo yao.


Nawe Yuda vilevile, nimekupangia wakati utakapovuna azabu.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Damasiki, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekatakata watu wa Gileadi wakitumia majembe ya mashini ya kulima.


Kati ya mataifa yote katika ulimwengu, ni ninyi tu niliowachagua. Kwa hiyo nitawaazibu ninyi, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.


Sanamu mutu aliyotengeneza inafaa kwa nini? Sanamu ni madini yaliyoyeyushwa, ni kitu cha kueneza udanganyifu! Mutengenezaji wa sanamu anatumainia kile alichotengeneza mwenyewe, sanamu ambayo haiwezi hata kusema!


Wanabadilisha ukweli juu ya Mungu kuwa uongo; wanaabudu na kutumikia vitu vilivyoumbwa kuliko Muumba mwenyewe, anayestahili kutukuzwa milele! Amina.


Basi kwa hiyo, yeye anayekataa mafundisho haya hamukatai mutu, lakini anamukataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mutakatifu.


Kwa maana munajua namna gani mulivyokombolewa toka katika tabia za ovyo ovyo mulizoambukizwa na babu zenu. Hamukukombolewa kwa njia ya vitu vinavyoharibika kama vile feza au zahabu.


Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ