Amosi 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Nilichagua manabii kati ya wana wenu, na wengine kati ya vijana wenu kuwa wanaziri. Enyi Waisraeli, haya ninayosema si ya kweli? –Ni ujumbe wa Yawe.–
Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”
na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.
Naye Yehu mwana wa Nimusi, umupakae mafuta akuwe mufalme wa Israeli. Elisha mwana wa Safati wa Abeli-Mehola, utamupakaa mafuta akuwe nabii kwa pahali pako.
Wakati uleule, nabii mumoja akamwendea Ahabu, mufalme wa Israeli, akamwambia: “Yawe anasema hivi: ‘Unaona wingi wa waaskari hawa? Leo hii nitawatia katika mikono yako, nawe utatambua kwamba mimi ndimi Yawe.’ ”
Naye mufalme wa Israeli akamujibu Yosafati: “Kungali mumoja, Mikaya mwana wa Imula. Yeye tunaweza kumwomba shauri la Yawe. Lakini ninamuchukia sana kwa sababu yeye, hatabiri jambo zuri juu yangu hata kidogo, lakini baya tu.” Yosafati akamwambia: “Si vizuri kwa mufalme kusema hivyo.”
Yawe alituma manabii na waonaji kuionya inchi ya Israeli na ya Yuda akisema: “Mwache njia zenu mbaya mutii amri zangu na masharti yangu kufuatana na sheria nilizowapa babu zenu, na ambazo niliwapa ninyi kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!
Kisha makuhani na manabii wakawaambia wakubwa na watu wote: Mutu huyu anastahili hukumu ya kifo, kwa maana ametabiri juu ya muji huu, kama vile ninyi wenyewe mulivyosikia kwa masikio yenu.
Vijana wa Sayuni walikuwa safi kuliko teluji, walikuwa weupe kuliko maziwa. Miili yao ilikuwa myekundu kuliko mawe ya matumbawe, uso wao kama jiwe la rangi ya samawi.
akiwaambia: “Tuliwakataza kwa nguvu musifundishe tena kwa jina la mutu huyu. Na sasa mumeeneza mafundisho yenu katika Yerusalema yote, nanyi munataka kutubebesha lazima ya kifo chake.”
Kwa hiyo Saulo akatuma watu kwenda kumukamata. Lakini walipokuta kundi la manabii likitabiri na Samweli akiliongoza, Roho wa Mungu aliwafikia wale watumishi wa Saulo, nao vilevile wakaanza kutabiri.
Watu wote katika inchi ya Israeli toka Dani, upande wa kaskazini, mpaka Beri-Seba, upande wa kusini, wakajua kwamba Samweli alikuwa nabii mwaminifu wa Yawe.