Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Nitavivunjavunja vifungio vya milango ya muji wa Damasiki, na kuwaondoa wakaaji wa bonde la Aweni, pamoja na mutawala wa Beti-Edeni. Waaramu wanapelekwa katika uhamisho kule Kiri. –Ni Yawe anayesema hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 1:5
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mambo mengine ya Yeroboamu, yote aliyofanya, vita alivyopigana kwa ushujaa, na jinsi alivyoikomboa Damasiki na Hamati na kuifanya mali ya Israeli, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.


Tigilati-Pileseri, akiitika kwa ombi la Ahazi, aliushambulia muji wa Damasiki na kuuteka. Akamwua mufalme Resini na kuwapeleka wafungwa kule Kiri.


Majeshi ya Elamu, pinde na mishale katika mikono, walikuja wamepanda farasi na magari ya vita; nalo jeshi la Kiri lilitayarisha ngao zake.


Yawe, Mukombozi wenu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: Kwa ajili yenu nitatuma waaskari kwenda Babeli. Nitavunja vifungio vya milango ya muji wake, na kelele za wale Wakaldea zitageuka maombolezo.


Maana mbele mutoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka neno “Baba” au “Mama”, utajiri wa muji wa Damasiki na vitu walivyonyanganya kule Samaria vitapelekwa kwa mufalme wa Asuria.


Upanga ukuwe juu ya waaguzi, kusudi wakuwe wapumbafu! Upanga ukuwe juu ya mashujaa, kusudi waangamizwe!


Waaskari wa Babeli wameshindwa kupigana, wamebaki katika makimbilio yao; nguvu zao zimewaishia, wamekuwa kama wanawake. Nyumba za Babeli zimechomwa kwa moto, milango yake ya chuma imevunjwa.


Milango yake imezama ndani ya udongo, ameharibu na kuvunjavunja vifungio vyake. Mufalme na wakubwa wake wako katika uhamisho kati ya mataifa. Hakuna sheria tena, manabii wake hawapati tena maono kutoka kwa Yawe.


Wakaaji wa miji ya Harani, Kane na Edeni na wachuuzi wa Asuria na Kilmadi walifanya biashara nawe.


Vijana wanaume wa Oni na Pibeseti watauawa kwa upanga, na wakaaji wengine watapelekwa katika uhamisho.


Pahali pa kutambikia juu ya vilima pa Aweni, pahali Waisraeli walipofanyia zambi, pataharibiwa. Miiba na michongoma vitaota katika mazabahu zao. Nao wataiambia milima: Mutufunike na vilima: Mutuangukie!


Lakini musinitafutie kule Beteli wala musiende Gilgali wala musivuke kwenda Beri-Seba. Maana wakaaji wa Gilgali, hakika watapelekwa katika uhamisho, na Beteli utaangamizwa!


Kwangu mimi, ninyi Waisraeli, muko sawasawa na watu wa Kushi! –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwatoa Wafilistini kutoka Krete, na Waaramu kutoka Kiri, kama nilivyowatoa ninyi kutoka Misri.


Angalia, waaskari wako ni wanawake tu. Milango ya inchi yako ni wazi mbele ya waadui zako; moto umeteketeza kabisa vifungio vyake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ