Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Basi, nitashusha moto juu ya nyumba ya mufalme Hazaeli, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za mufalme Beni-Hadadi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 1:4
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia: “Urudie kwa kupitia njia ya jangwa mpaka Damasiki. Utakapofika, umupakae Hazaeli mafuta akuwe mufalme wa Aramu.


Mufalme Yoasi akamushinda Beni-Hadadi mara tatu na kuikomboa miji yote iliyotekwa wakati wa utawala wa Yoahazi, baba ya Yoasi.


Yawe alikasirika, akawafanya watu wa Israeli washindwe katika vita mara kwa mara na mufalme Hazaeli wa Aramu na mwana wake Beni-Hadadi.


Nyuma ya hayo, mufalme Beni-Hadadi wa Aramu akakusanya waaskari wake wote akatoka na kuuzunguka muji wa Samaria.


Kwa hiyo mufalme Asa akatwaa feza na zahabu kutoka katika hazina ya nyumba ya Yawe na ya nyumba ya kifalme, akazituma Damasiki kwa Beni-Hadadi, mufalme wa Suria, na ujumbe akasema:


Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitawasha moto katika kuta za Damasiki, nao utateketeza nyumba nzuri za mufalme Beni-Hadadi.


Nitakapoiteketeza Misri kwa moto na kuvunjavunja wasaidizi wake wote, halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitawasha moto juu ya inchi ya Magogi na juu ya wote wanaokaa salama katika inchi za kandokando ya bahari. Nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Tiro, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.


Basi, nitashusha moto juu ya muji wa Temani, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Bosira.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Raba, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri. Siku hiyo ya vita kutakuwa makelele mengi, nayo mapambano yatakuwa makali kama zoruba.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Gaza, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.


Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Moabu, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za muji wa Kerioti. Waaskari watakapolalamika kwa sauti zao na kupiga baragumu, watu wa Moabu watakufa katika makelele hayo ya vita.


Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Yuda, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Yerusalema.


Vilevile Mungu akawafanya watu wa Sekemu waazibiwe kwa uovu wao walioufanya. Hivyo, laana ya Yotamu mwana wa Yerubali ikawapata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ