Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Basi, nitashusha moto juu ya muji wa Temani, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Bosira.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 1:12
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.


Bela alipokufa, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosira akatawala pahali pake.


Upanga wa Mungu uko tayari juu mbinguni. Angalia, unashuka kuwaazibu Waedomu, watu ambao ameamua kuwaangamiza.


Upanga utajaa damu na mafuta: damu ya kondoo na mbuzi, na mafuta ya figo za kondoo dume. Maana Yawe ana sadaka huko Bosira, kutakuwa mauaji makubwa katika inchi ya Edomu.


Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosira na nguo ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa nguo ya utukufu, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Yawe ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.


Maana nimeapa kwa nafsi yangu kwamba muji wa Bosira utakuwa kitisho na mushangao, utakuwa uharibifu na kutumiwa kama mufano wa laana; vijiji vyote vitakuwa mabomoko siku zote. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hiyo, musikilize mupango ambao mimi Yawe nimepanga juu ya Edomu pamoja na mambo niliyokusudia kuwafanyia wakaaji wa Temani: Hakika, watoto wao wadogo watakokotwa na kukamatwa; kweli kutakuwa mushangao mukubwa katika makao yao!


Adui atapanda juu na kuruka kama tai na kutandaza mabawa yake juu ya Bosira. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Edomu utakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.


Juu ya Edomu, Yawe wa majeshi anasema hivi: Hakuna tena hekima katika muji wa Temani? Wenye hekima wao hawana shauri tena? Hekima imetoweka kabisa?


basi, Bwana wetu Yawe anasema: Nitanyoosha mukono juu ya inchi ya Edomu kwa kuwaazibu na kuwaua watu wote na nyama. Nitaifanya kuwa ukiwa kutoka muji wa Temani mpaka muji wa Dedani. Watu wa inchi hiyo watauawa kwa upanga.


Haya ni maono ya Obadia. Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya taifa la Edomu. Tumepata habari kutoka kwa Yawe; mujumbe ametumwa kati ya mataifa: Musimame! Tuende tupigane na taifa la Edomu!


Mungu amekuja kutoka jimbo la Temani, Mungu mutakatifu anakuja kutoka mulima Parani. Utukufu wake umeenea pote mbinguni, nayo dunia imejaa sifa zake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ