Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




3 Yoane 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwa maana hawa walianza safari yao kwa ajili ya kazi ya Kristo bila kupokea musaada wowote toka kwa watu wasioamini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




3 Yoane 1:7
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini watawafanyia ninyi haya yote kwa ajili yangu, kwa sababu hawamujui yule aliyenituma.


Mimi sikutamani feza, zahabu, wala nguo ya mutu yeyote.


Katika mambo hayo yote niliyofanya, nimewaonyesha mufano kwamba tunapaswa kusumbuka vile na kazi kwa kuwasaidia wasiojiweza, tukikumbuka maneno haya Bwana Yesu mwenyewe aliyosema: ‘Ni heri kutoa kuliko kupewa.’ ”


Basi mitume wakatoka katika baraza, wakifurahi sana kwa sababu walistahili kuzarauliwa kwa kuteswa kwa ajili ya Yesu.


Wale waamini waliosambaa walikwenda popote wakitangaza Habari Njema.


Nami nitamwonyesha mateso ya namna gani atakayopaswa kupata kwa ajili yangu.”


Basi mushahara wangu ni gani? Mushahara wangu ni kutangaza Habari Njema bila kulipwa, maana yake bila kudai haki ninazostahili kwa kuitangaza.


Mumepungukiwa na nini kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi sikuwalemea kwa kupata musaada toka kwenu? Munisamehe kwa kosa hili.


Kwa maana, hatutangazi habari zetu sisi wenyewe, lakini tunatangaza kwamba Yesu Kristo ndiye Bwana, nasi tuko watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.


Kwa hiyo Mungu naye akamwinua juu zaidi, akamupa jina lenye ukubwa kuliko majina yote,


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Basi sisi tunapaswa kuwasaidia watu kama hawa tupate kushiriki pamoja nao katika kazi ya kutangaza ukweli.


Wewe ni muvumilivu; umeteswa kwa ajili ya jina langu, lakini haukuregea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ