Naye Yawe atatimiza ahadi yake aliyotoa aliponiambia kwamba, ikiwa wazao wangu watatii amri zake na kumutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wote, hakutakosekana mumoja wao kwa kutawala Israeli nyakati zote.
Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.
“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.
akisema: Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote, na kutenda mazuri mbele yako. Hezekia akalia kwa uchungu sana.
Wakati nilipoona kwamba walikuwa wakitembea kinyume cha ukweli wa Habari Njema, nikamwambia Petro hivi mbele ya watu wote: “Ikiwa wewe unayekuwa Muyuda unafuata desturi za watu wa mataifa mengine, namna gani unaweza kuwalazimisha watu wa mataifa mengine wafuate desturi za Wayuda?”
Watoto wangu wapendwa, kama vile mwanamuke anavyopata uchungu wa kuzaa, mimi vilevile, ninapata tena uchungu kwa ajili yenu mpaka mutakapokuwa na hali inayokuwa kama ya Kristo ndani yenu.
Ninakuandikia wewe Timoteo mwana wangu wa kweli katika imani. Ninakutakia neema na rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
Watoto wangu wapendwa, ninawaandikia maneno hayo kusudi musitende zambi. Lakini kama mutu akitenda zambi, tuko na yule anayetutetea mbele ya Baba. Naye muteteaji yule ndiye Yesu Kristo, mwenye haki.