Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




3 Yoane 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




3 Yoane 1:11
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, uache kusema mabaya, na kuepuka kusema uongo.


Achana na uovu, utende mazuri, nawe utaishi katika inchi siku zote;


Usifuate watu wengi kwa kutenda ubaya. Wala wakati wa kukata maneno, usishuhudie kufuatana na watu wengi kwa kupotosha haki.


Mulimaji mwenye bidii ana chakula tele, lakini anayefuata mambo yasiyofaa hana akili.


Kondoo wangu wanasikia sauti yangu, ninawajua, nao wananifuata.


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Kila mutu anayefanya mabaya anachukia mwangaza, naye anakataa kuja kwenye mwangaza, kusudi matendo yake yasionekane wazi.


Mufuate mufano wangu kama vile mimi ninavyofuata mufano wa Kristo.


Mufuate tabia ya Mungu kwa maana ninyi ni watoto wake wapendwa.


Wandugu zangu, mufuate mufano wangu, muwaangalie vizuri wale wanaofuata mwenendo muliouona kwetu.


Ninyi mumefuata mufano wetu na mufano wa Bwana, kwa kuwa ingawa muliteswa sana, mulipokea neno la Mungu kwa furaha inayotoka kwa Roho Mutakatifu.


Wandugu, mambo yale yale yaliyotokea makanisa ya Mungu ya Yudea yanayoungana na Yesu Kristo, ndiyo yaliyowatokea ninyi vilevile. Kwa maana ninyi muliteswa na wanainchi wenzenu kama vile wao walivyoteswa na wanainchi wenzao Wayuda.


Lakini wewe umefuata kabisa mufano wangu katika mafundisho yangu na mwenendo wangu, makusudi yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, ungojevu wangu,


Basi musigeuke kuwa wavivu, lakini mufuate mufano wa wale wanaoamini na kuvumilia. Kwa njia hiyo wanapokea yale Mungu aliyoahidi kuwapa.


Aepuke mabaya, atende mema, atafute amani na kuifuatilia.


Ni nani atakayewazuru ninyi kama mukiwa wenye bidii katika kutenda mema?


Munajua kwamba Kristo ni mwenye haki, kwa hiyo munapaswa kujua vilevile kwamba kila mutu anayefuata haki ni mutoto wa Mungu.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ