Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.
Mafundisho yao yalikuwa ya kweli nao hawakufundisha uongo hata kidogo. Mimi na wao tulikaa kwa amani. Si kwamba walitenda haki tu, lakini waliwafundisha wengine kutotenda maovu.
Wakati nilipoona kwamba walikuwa wakitembea kinyume cha ukweli wa Habari Njema, nikamwambia Petro hivi mbele ya watu wote: “Ikiwa wewe unayekuwa Muyuda unafuata desturi za watu wa mataifa mengine, namna gani unaweza kuwalazimisha watu wa mataifa mengine wafuate desturi za Wayuda?”
Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.
Nilipata furaha kubwa katika kuungana na Bwana kwa kuona munakumbuka tena kunisaidia. Sitaki kusema kwamba mulinisahau, lakini hamukupata wakati wa kuonyesha kwamba munanishugulikia.