Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Yoane 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Nina maneno mengi ya kuwaambia, lakini sitaki kuyaandika ndani ya barua. Ninatumaini nitawatembelea na kusemezana pamoja nanyi uso kwa uso, kusudi tupate kujazwa na furaha kabisa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Yoane 1:12
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi ninaongea naye kinywa kwa kinywa, waziwazi na si kwa kutumia mafumbo. Yeye ameliona umbo langu mimi Yawe. Kwa nini, basi, hamukuogopa kusema vibaya juu ya mutumishi wangu Musa?


“Nimewaambia ninyi maneno haya kusudi mufurahi sawa mimi, na furaha yenu ikuwe kubwa kabisa.


“Ningali na maneno mengi ya kuwaambia, lakini sasa hamujakuwa na uwezo wa kuyafahamu.


Mpaka sasa hamujaomba kitu kwa jina langu. Muombe, nanyi mutapewa, na furaha yenu itakuwa kubwa kabisa.


Lakini sasa ninarudi kwako, nami ninasema maneno haya nikingali katika dunia, kusudi furaha yangu kubwa kabisa ikuwe ndani yao.


Mwenye bibi arusi ndiye bwana-arusi; lakini rafiki ya bwana arusi anasimama karibu naye na kumusikiliza, anafurahi sana kusikia sauti ya bwana-arusi. Na ni hivi mimi ninafurahi, na furaha yangu imetimia sasa.


kwa hiyo nitawafikia nitakapokwenda Spania. Ninatumaini kupitia kule na kuonana nanyi, na kisha kufurahi kwanza pamoja nanyi kwa muda mufupi, ningetamani kupata musaada wenu kwa ajili ya safari ile.


Nikikumbuka machozi yako, ninatamani sana kukuona kusudi nipate kujazwa na furaha.


Lakini pamoja na maneno haya, unitayarishie vilevile pahali pa kukaa, maana ninatumaini kwamba Mungu atajibu maombi yenu, na kunijalia nipate kurudishwa tena kwenu.


Ninawasihi sana kuomba Mungu, kusudi nipate kurudishwa kwenu upesi.


Ninapenda kuwajulisha kwamba ndugu yetu Timoteo amekwisha kufunguliwa. Kama akikuja upesi, nitafika kuwaona pamoja naye.


Tunawaandikia ninyi maneno haya kusudi tupate kujazwa na furaha kabisa.


Kwa sababu hiyo wakati nitakapokuja, nitaonyesha wazi mambo yote anayotenda akitusingizia sisi maneno mabaya. Lakini hatosheki na mambo yale, yeye mwenyewe anakataa kukaribisha wandugu wale wanaokuwa katika safari. Na wale wanaotaka kuwakaribisha, anawakataza na kuwafukuza katika kanisa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ