Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 9:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 9:7
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe unapima moyo, nawe unapendezwa na uaminifu. Nami, katika uaminifu wa moyo wangu nimetoa vitu hivi vyote kwa mapenzi yangu, na sasa ninaona watu wako wanaokuwa hapa, wakikutolea kwa mapenzi yao na furaha.


Halafu watu wakafurahi kwa sababu walitoa kwa mapenzi yao, maana kwa moyo wao wote walimutolea Yawe kwa mapenzi yao, naye mufalme Daudi akafurahi sana.


Uwaambie Waisraeli wanipe michango ya matoleo. Utapokea matoleo kutoka kwa mutu yeyote atakayetoa kwa moyo safi.


Mutatoa katika mali zenu muchango wa kumupa Yawe. Kila mutu mwenye moyo mwema atamuletea Yawe muchango: sadaka, feza, shaba;


Mutu anayetoa kwa moyo safi atafanikishwa. Mutu anayekunywesha mwingine maji, naye atakunyweshwa.


Mutu mwenye kuwa tayari kusaidia atabarikiwa, maana anagawanya chakula chake na masikini.


Wapumbafu hawataitwa tena wenye cheo, wala watu wa ovyoovyo hawataitwa tena waheshimiwa.


Lakini wenye heshima wanatenda mambo ya heshima, nao wanatetea mambo yenye heshima.


Katika mambo hayo yote niliyofanya, nimewaonyesha mufano kwamba tunapaswa kusumbuka vile na kazi kwa kuwasaidia wasiojiweza, tukikumbuka maneno haya Bwana Yesu mwenyewe aliyosema: ‘Ni heri kutoa kuliko kupewa.’ ”


Aliyepewa zawadi ya kuonya wengine, awaonye. Aliyepewa zawadi ya kutoa, atoe kwa moyo mweupe. Anayesimamia wengine, awasimamie kwa bidii. Aliyepewa zawadi ya kuhurumia wengine, afanye vile kwa furaha.


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Umupe kwa moyo safi kile ambacho Yawe amekubariki nacho: kondoo, ngano na divai.


Lakini sikutaka kufanya kitu chochote pasipo shauri lako. Wala sikutaka kukulazimisha unitendee mema; lakini ningetaka uyatende kwa mapenzi yako mwenyewe.


Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango!


Mukaribishane ninyi kwa ninyi pasipo kunungunika.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ