Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 9:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Ni hivi niliona kuwa ni vizuri kuwashauri wandugu hawa watangulie kufika kwenu mbele yangu kusudi watayarishe vile vitu mulivyoahidi kutoa kwa mapenzi yenu. Hivi vitakuwa tayari na itaonyesha kwamba mumevitoa kwa moyo mwema, wala si kwa uchoyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 9:5
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, ninakuomba ukubali zawadi niliyokuletea, kwa sababu hata mimi vilevile Mungu amenineemesha, nami nina mali nyingi.” Ndivyo Yakobo alivyomushawishi Esau, naye akapokea zawadi yake.


Halafu akarudi kwa mutu wa Mungu pamoja na watu wake, akasema: “Sasa ninajua kwamba hakuna Mungu yeyote katika dunia lakini tu Mungu wa Israeli; kwa hiyo, tafazali sasa upokee zawadi ya mutumishi wako.”


Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.


Ni kwa hiyo tulimusihi Tito atimize kazi hiyo ya kuwaongoza ninyi kuwa na moyo wa kutoa sawa alivyoianzisha.


Lakini sasa ninawatumia wandugu hawa kusudi kujisifu kwetu kwa ajili yenu kusionekane kuwa bure. Kwa hiyo ninataka mukuwe tayari kama vile nilivyosema.


Mukumbuke maneno haya: yule anayepanda kidogo atavuna kidogo, na yule anayepanda kwa uwingi atavuna kwa uwingi.


Sitaki kusema kwamba ninatafuta tu kupokea zawadi, lakini ninataka faida iongezwe kwa upande wenu.


Akamujibu: “Unipe zawadi! Ninaomba unipe chemichemi za maji maana kule upande wa kusini ni jangwa.” Kalebu akamupa chemichemi za upande wa juu na za chini.


Bwana wangu, ninakuomba upokee zawadi hii niliyokuletea, na uwape vijana wanaokufuata.


Daudi aliporudia Ziklagi, aliwapelekea warafiki zake ambao ni wazee wa Yuda sehemu ya vitu akisema: “Ninawaletea zawadi kutoka katika vitu vya waadui wa Yawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ