Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 8:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 8:9
43 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.


Kwa ajili ya Sayuni sitakaa kimya, kwa ajili ya Yerusalema sitatulia, mpaka kuokolewa kwake kuonekane kama umeme, wokovu wake utokee kama mwangaza.


Yawe anasema hivi: Mutu akikuta kishada cha mizabibu mizuri, watu wanasema: Tusikiharibu; kina baraka. Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.


Lakini haifai kuwakwaza. Kwa hiyo kwenda kwenye ziwa, na utupe ndoana ndani ya maji. Na samaki wa kwanza utakayemunasa, ufungue kinywa chake, nawe utaona kikoroti cha feza. Ukikamate na kukitoa kwa kulipa kodi kwa ajili yetu sisi wawili.”


Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


Yesu akamujibu: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu, nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”


Huyu si yule museremala, mwana wa Maria, ndugu ya Yakobo, Yose, Yuda na Simoni? Nao wadada zake, si wanaishi hapa kati yetu?” Na kwa hiyo wakakosa kumwaminia.


Basi kama ninyi hamukukuwa waaminifu kwa kulinda mali ya dunia hii, ni nani atakayeweza kuwatumainia kwa kulinda mali ya kweli?


Akazaa mwana, ndiye muzaliwa wake wa kwanza. Akamufunika nguo za kitoto na kumulalisha katika sanduku ya kukulishia nyama, kwa sababu walikosa nafasi ya kukaa katika nyumba ya kupangisha wageni.


na Yoana muke wa Kuza, huyo mume wake alikuwa musimamizi wa mali ya Herode, pamoja na Suzana na wengine wengi. Wanawake hawa walitumia mali yao kwa kuwasaidia Yesu na wanafunzi wake.


Yesu akamwambia: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”


Neno alikuwa yuko katika dunia, nayo dunia iliumbwa kwa njia yake, lakini ijapokuwa vile haikumutambua.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo.


Lakini Yesu akawaambia: “Sauti hii haikusikilika kwa ajili yangu, lakini kwa ajili yenu.


Yote Baba anayokuwa nayo ni yangu. Ni kwa sababu hii nilisema kwamba maneno Roho atakayowaambia yatatokana na yale yanayokuwa ndani yangu.


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Kosa lao limeiletea dunia baraka nyingi, na upungufu wao umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengi. Basi haitaleta baraka zaidi sana wakati Waisraeli wote watakapookoka?


Kwa maana hata Kristo hakufanya mambo yanayomupendeza mwenyewe sawa vile ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Matusi wanayokutukana, yananiangukia.”


Lakini Mungu ameonyesha wazi upendo wake kwetu ni wapata gani, kwa maana tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Ninamushukuru Mungu wangu siku zote kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema Mungu aliyowapa ninyi kwa njia ya Yesu Kristo.


Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, yeye ni wa dunia, lakini Adamu wa pili alitoka mbinguni.


tunahuzunishwa lakini tunafurahi siku zote. Tunaonekana kama wamasikini lakini tunatajirisha watu wengi, hatuna kitu, lakini tunakuwa na vitu vyote.


Alifanya vile kusudi aonyeshe kwa vizazi vyote vitakavyokuja neema yake kubwa ya ajabu kwa njia ya wema wake katika kuungana kwetu na Yesu Kristo.


Mutafikia kweli kutambua upendo wake, ijapokuwa unapita ufahamu wa watu wote, nanyi mutapata kuwa watimilifu kabisa sawa vile Mungu anavyokuwa.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Uwaagize watende mema, wakuwe watajiri katika matendo mazuri, nao wasaidiane kwa moyo safi na kushiriki mali yao na wengine.


Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Ninajua mateso yako na umasikini wako, lakini wewe ni tajiri! Vilevile ninajua jinsi unavyotukanwa na wale wanaojidai kuwa Wayuda lakini si Wayuda; wao ni kikundi cha wenye kuabudu Shetani!


Yule atakayeshinda atapokea toka kwangu zawadi ile, mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ