Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yalitusihi sana tukishiriki nayo katika kazi ya kuwasaidia watu wa Mungu wanaokaa Yudea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 8:4
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”


Kwa maana yeyote anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa katika mbingu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Kwa maana mutakuwa na wamasikini pamoja nanyi siku zote, na munaweza kuwasaidia wakati wowote munapotaka, lakini mimi sitakuwa pamoja nanyi siku zote.


Wanafunzi wakakusudia kutuma musaada kwa wandugu waamini waliokaa katika jimbo la Yudea, kila mumoja kwa kadiri alivyoweza kutoa.


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


“Nyuma ya kupitisha miaka mingi mbali na muji, nilirudi kule Yerusalema kuwaletea watu wa taifa langu musaada wa mali na kumutolea Mungu sadaka.


Muniombee kusudi nisipate hasara toka kwa watu wale wasioamini wanaokuwa Yudea na kusudi musaada ninaoupeleka Yerusalema upate kupokelewa vizuri kule na watu wa Mungu.


Sasa juu ya muchango unaofanyika kwa ajili ya watu watakatifu wa Mungu wanaokuwa Yerusalema; ninyi vilevile mufanye sawa vile nilivyoagiza makanisa ya Galatia.


Ninyi munajua Stefana na jamaa yake; munafahamu kwamba walikuwa watu wa kwanza walioamini katika inchi ya Akaya, nao wamejitoa kwa kutumikia watu wa Mungu. Hivi ninawasihi sana wandugu zangu,


Si lazima niwaandikie juu ya musaada unaotumwa kwa watu wa Mungu wanaokuwa katika Yudea.


Lakini kitu kimoja walichotuomba ni kukumbuka wamasikini wa makanisa yao, nami nimefanya vile kwa bidii.


Basi, tunapokuwa bado na wakati, tufanye mema kwa watu wote, na zaidi kwa wandugu zetu katika imani.


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ