Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 8:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 8:12
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yawe alimwambia baba yangu Daudi: ‘Ni vizuri kwamba ulikusudia ndani ya moyo wako kunijengea nyumba.


Uwaambie Waisraeli wanipe michango ya matoleo. Utapokea matoleo kutoka kwa mutu yeyote atakayetoa kwa moyo safi.


Kila mutu aliyeweza kutoa feza au shaba aliileta kwa Yawe kama matoleo yake. Tena mutu yeyote aliyekuwa na mbao za mujohoro alileta vilevile.


Waisraeli wote, wanaume na wanawake, ambao walivutwa ndani ya moyo wao kuleta kitu chochote kwa ajili ya kazi ambayo Yawe alikuwa amemwagiza Musa ifanyike, walileta vitu hivyo kwa mapenzi yao, kama vile muchango wa kumupa Yawe.


Mutatoa katika mali zenu muchango wa kumupa Yawe. Kila mutu mwenye moyo mwema atamuletea Yawe muchango: sadaka, feza, shaba;


Kitu kinachotakiwa kwa mutu ni uaminifu; afazali mutu masikini kuliko mutu mwongo.


Na yule aliyepata furushi mbili akafaidia zingine mbili.


Halafu mutumishi aliyepewa furushi mbili akakuja, akasema: ‘Bwana, umenipatia furushi mbili; na sasa angalia, kuna faida ya zingine mbili.’


Yule anayekuwa mwaminifu katika vitu vichache, yuko mwaminifu vilevile katika vitu vingi. Na yule asiyekuwa mwaminifu katika vitu vichache, hayuko mwaminifu vilevile katika vitu vingi.


Sasa muendelee nayo na kuitimiza. Kama vile mulivyokuwa na moyo mwema wa kukusudia kuifanya, basi mukuwe na moyo mwema wa kuitimiza kufuatana na uwezo wa mali munayokuwa nayo.


Nia yangu si kusema kwamba munapaswa kujitia katika taabu kwa ajili ya kusaidia watu wengine, lakini inafaa kuwe usawa.


Vilevile, yule ndugu amechaguliwa na makanisa kwa kutusindikiza katika safari ya kutimiza kazi hii ya kutoa kwa moyo mwema ambayo sisi tunafanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana, na kwa kuonyesha nia yetu ya kusaidia watu wengine.


Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.


Kila mutu kati yenu anapaswa kuitumia zawadi ya kiroho aliyojaliwa na Mungu kwa ajili ya mafaa ya wengine. Na hivi mutakuwa walinzi wazuri wa zawadi mbalimbali mulizopewa na Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ