2 Wakorinto 8:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Kuelekea jambo hilo, mimi ninawatolea shauri, nalo linafaa kwenu, kwa maana ni ninyi muliokuwa wa kwanza kukusudia kufanya kazi ile na kuianzisha tangu mwaka jana.
Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”
Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.
Wamoja kati yenu wanasema: “Vitu vyote vinaruhusiwa kwangu.” Ndiyo, lakini vyote si vyenye kufaa kwenu. Ninaweza kusema kwamba vitu vyote vinaruhusiwa kwangu, lakini sitakubali kuwa mutumwa wa kitu chochote.
Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mutu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana.
Sisemi hivi kwa kuwaamuru, lakini kwa njia ya kuwaelezea habari za bidii ya wengine, ninataka kuwapima kusudi upendo wenu upate kutambulikana kuwa wa kweli.
Kwa maana ninajua nia yenu nzuri ya kusaidia, nami ninajivuna kwa ajili yenu mbele ya watu wa Makedonia, nikisema: “Kanisa la jimbo la Akaya liko tayari kusaidia tangia mwaka jana.” Hivi kwa njia ya bidii yenu mumewavuta wengi kati yao kwa kutoa vilevile.