Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 8:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kuelekea jambo hilo, mimi ninawatolea shauri, nalo linafaa kwenu, kwa maana ni ninyi muliokuwa wa kwanza kukusudia kufanya kazi ile na kuianzisha tangu mwaka jana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 8:10
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”


Hamufahamu kwamba ni afazali mutu mumoja akufe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima kuangamizwa?”


Lakini mimi ninawaambia ukweli: ni faida kwenu mimi niende, kwa maana nisipokwenda, Musaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, nitamutuma kwenu.


Ni Kayafa aliyewashauria Wayuda kwamba ni afazali mutu mumoja akufe kwa ajili ya watu wote.


Wamoja wenu wanasema: “Vitu vyote vinaruhusiwa.” Ni kweli, lakini vyote havifai. “Vitu vyote vinaruhusiwa,” lakini vyote havifai kwa kujenga imani.


Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.


Wamoja kati yenu wanasema: “Vitu vyote vinaruhusiwa kwangu.” Ndiyo, lakini vyote si vyenye kufaa kwenu. Ninaweza kusema kwamba vitu vyote vinaruhusiwa kwangu, lakini sitakubali kuwa mutumwa wa kitu chochote.


Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mutu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana.


Lakini ingekuwa heri zaidi kama angekaa sawa vile anavyokuwa. Hilo ni shauri langu, nami vilevile ninazani kwamba ninaongozwa na Roho wa Mungu.


Basi nitaendelea kujivuna ijapokuwa si vizuri. Lakini nitasema sasa juu ya maono na ufunuo nilivyopata toka kwa Bwana.


Ni kwa hiyo tulimusihi Tito atimize kazi hiyo ya kuwaongoza ninyi kuwa na moyo wa kutoa sawa alivyoianzisha.


Sisemi hivi kwa kuwaamuru, lakini kwa njia ya kuwaelezea habari za bidii ya wengine, ninataka kuwapima kusudi upendo wenu upate kutambulikana kuwa wa kweli.


Kwa maana ninajua nia yenu nzuri ya kusaidia, nami ninajivuna kwa ajili yenu mbele ya watu wa Makedonia, nikisema: “Kanisa la jimbo la Akaya liko tayari kusaidia tangia mwaka jana.” Hivi kwa njia ya bidii yenu mumewavuta wengi kati yao kwa kutoa vilevile.


Sitaki kusema kwamba ninatafuta tu kupokea zawadi, lakini ninataka faida iongezwe kwa upande wenu.


Tena, musisahau kutenda mema na kusaidiana, maana sadaka za namna hii zinamupendeza Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ