Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 7:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Nasi hatukufarijiwa kwa kuja kwake tu, lakini vilevile kwa namna ile mulivyomufariji. Tito ametuelezea jinsi munavyokuwa na hamu kubwa ya kuniona, jinsi munavyohuzunika na jinsi munavyojitoa kwa ajili yangu. Kwa hivi sasa ninafurahi zaidi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 7:7
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.


Mumwimbie Yawe sifa, enyi waaminifu wake; mukumbuke utakatifu wake na kumushukuru.


Mimi ni karibu ya kuanguka; ninakuwa na maumivu ya siku zote.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi inayoelekea wakati nabii Natani alipomufikia kwa kumwonya juu ya uzinzi alioufanya na Batiseba.


naye Petro akakumbuka maneno yale Yesu aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika, atakuwa amemukana mara tatu. Basi akatoka inje, akalia kwa uchungu sana.


Heri wale wanaokuwa na huzuni, maana Mungu atawafariji!


Yesu alikuwa katika uchungu mukubwa, akazidi kuomba kwa bidii. Jasho iliyomutoka ikakuwa kama matone ya damu yaliyokuwa yakitiririka mpaka chini.]


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Ni kusema kwamba nipate kutiwa moyo kwa njia ya imani yenu na ninyi kwa njia ya imani yangu.


Nanyi munajaa na kiburi. Ninyi mungepaswa kuhuzunika na mutu yule aliyefanya kile kitendo, naye angepaswa kutengwa toka katikati yenu.


maana munayafahamu sasa kwa sehemu tu. Kwa Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu mutaweza kujivuna kwa ajili yetu kama vile tutakavyojivuna kwa ajili yenu.


Yeye anatufariji katika taabu yetu yote, kusudi tupate kuwafariji wale wanaokuwa katika taabu yoyote kwa kuwaletea faraja tuliyopokea kutoka kwa Mungu.


Kwa maana shabaha yangu ya kuwaandikia ile barua ni kutaka kuwapima nipate kujua kwamba muko tayari kunitii siku zote.


Na sasa katika hali hii tunaugua kwa maana tunatamani sana kuvaa makao yetu yanayotoka mbinguni.


Lakini Mungu anayefariji watu wanyenyekevu, ametufariji kwa njia ya kufika kwa Tito.


Basi, ikiwa nimewahuzunisha na barua yangu, sijuti juu yake sasa. Nilijuta wakati nilipotambua kwamba barua ile iliwahuzunisha ingawa ilikuwa ni kwa muda tu.


Shukrani kwa Mungu aliyemutia Tito bidii ya kuwasaidia kama vile sisi tunavyokuwa nayo!


Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.


Ijapokuwa mimi ni mbali nanyi kwa mwili, lakini mimi ni pamoja nanyi kwa roho, nami ninafurahi kuona namna munavyoishi katika utaratibu muzuri na kusimama imara katika imani mbele ya Kristo.


Lakini sasa Timoteo amefika kwetu, akirudia toka kule kwenu. Ametuletea habari nzuri juu ya imani yenu na upendo wenu. Ametuelezea kwamba munatukumbuka vizuri siku zote, na kwamba muko na hamu sana ya kutuona, kama vile sisi nasi tunavyokuwa na hamu ya kuwaona.


Kwa maana sasa tunaweza kupumua kwa kuona munasimama imara katika kuungana kwenu na Bwana.


Kwa sababu hiyo, tunapaswa kushikamana zaidi na habari tuliyosikia, kusudi tusipotee mbali.


Elia alikuwa mutu kama sisi. Yeye aliomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya inchi kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Nilifurahi sana kuona kwamba wamoja kati ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama vile Baba alivyotuamuru.


Wapendwa wangu, wakati nilipokuwa nikifanya bidii sana ya kuwaandikia juu ya wokovu tunaoshiriki wote pamoja, nikaona sherti niwaandikie na kuwaonya mupate kutetea imani ile Mungu aliyotoa mara moja tu kwa watu wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ