2 Wakorinto 7:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
5 Kwa maana hata wakati tulipofika Makedonia, hatukuweza kupumzika hata kidogo. Tulipata taabu pande zote: magomvi pamoja na watu wengine, na woga katika moyo wetu.
Lakini kwa vile maji yalikuwa yangali yakifunika inchi yote, yule njiwa hakupata pahali pa kutua, akarudilia Noa katika chombo. Noa akanyoosha mukono, akamutwaa na kumurudisha ndani ya chombo.
Ninasikia watu wengi wakinisingizia uongo, nao wananipanga jina la Kitisho Kila Pahali! Wengine wanasema: Tumushitaki, Tumushitaki! Rafiki zangu wapenzi wote wanangojea kwa hamu nianguke! Wanasema: Labda atadanganyika, tupate kumunasa na kumulipiza kisasi.
Wandugu zangu, kila siku ninapatwa na hatari ya kufa. Na hii ni hakika sawa vile ninavyojivuna kwa ajili yenu katika kuungana kwangu na Yesu Kristo Bwana wetu.
Ni kwa sababu hii niliwaandikia kwamba sitakuja tena kwenu nisihuzunishwe na watu waliopaswa kunifurahisha. Maana nina uhakika kwamba mimi ninapofurahi, ninyi wote munafurahi vilevile.
Ni kwa sababu hiyo, nilipoona kwamba siwezi kuendelea kungojea, nilimutuma Timoteo kusudi nipate kujua habari ya imani yenu. Niliogopa kwamba labda yule mushawishi Shetani amejaribu kuwaangusha ninyi na kwamba kazi yote tuliyofanya kwenu imepotea bure.