2 Wakorinto 7:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Hii ndiyo maana tumefarijiwa. Lakini zaidi ya kufarijiwa kwetu tulifurahi tena sana kwa ajili ya furaha Tito aliyokuwa nayo kufuatana na jinsi mulivyomutuliza.
Ni kwa sababu hii niliwaandikia kwamba sitakuja tena kwenu nisihuzunishwe na watu waliopaswa kunifurahisha. Maana nina uhakika kwamba mimi ninapofurahi, ninyi wote munafurahi vilevile.
Mimi nimejivuna kidogo mbele yake kwa ajili yenu, nami sikupata haya. Lakini kama vile tulikuwa tunawaambia kila mara ukweli, vilevile kule kujisifu kwetu kwa ajili yenu mbele ya Tito, kumeonekana kuwa kwa kweli.