Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 7:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Hii ndiyo maana tumefarijiwa. Lakini zaidi ya kufarijiwa kwetu tulifurahi tena sana kwa ajili ya furaha Tito aliyokuwa nayo kufuatana na jinsi mulivyomutuliza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 7:13
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Na hivi Mungu akitaka, nitakuja kwenu kwa furaha, nami nitapata kutulizwa moyo kati yenu.


Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.


Mukeshe, musimame imara katika imani, mukuwe hodari na wenye nguvu.


nao wamenifariji kama vile walivyowafariji ninyi wenyewe. Inafaa kuwakumbuka watu kama hawa.


Ingawa vile, nilifazaika sana kwa sababu sikumukuta ndugu yangu Tito. Halafu nikaagana na watu wa muji ule na kwenda Makedonia.


Ni kwa sababu hii niliwaandikia kwamba sitakuja tena kwenu nisihuzunishwe na watu waliopaswa kunifurahisha. Maana nina uhakika kwamba mimi ninapofurahi, ninyi wote munafurahi vilevile.


Mimi nimejivuna kidogo mbele yake kwa ajili yenu, nami sikupata haya. Lakini kama vile tulikuwa tunawaambia kila mara ukweli, vilevile kule kujisifu kwetu kwa ajili yenu mbele ya Tito, kumeonekana kuwa kwa kweli.


Mapendo yake kwa ajili yenu yanazidi kuongezeka anapokumbuka vile mulivyokuwa tayari kumutii na vile mulivyomupokea kwa woga na kutetemeka.


Lakini Mungu anayefariji watu wanyenyekevu, ametufariji kwa njia ya kufika kwa Tito.


Hivi ninamutuma kwenu kwa haraka kusudi mupate kufurahi wakati mutakapomwona tena na huzuni yangu ipate kupunguka.


Bwana awajalie mema sana watu wa jamaa ya Onesiforo, kwa maana amekuja mara nyingi kunifariji, wala hakusikia haya kwa kuniona niko katika kifungo.


Ndiyo, ndugu yangu, ninakusihi unisaidie kwa njia hii kwa ajili ya Bwana, unitulize moyo kama vile ndugu katika Kristo.


Ndugu, upendo wako umenifurahisha sana na kunifariji, kwa maana umetuliza mioyo ya watu wa Mungu.


Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ