Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 7:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Basi, muangalie sasa matokeo ya ile huzuni inayosababishwa na Mungu! Imewafanya kuwa wenye bidii sana, wenye kujitetea, wenye kuonyesha kwamba hamuna kosa, wenye utii, wenye hamu kubwa ya kuniona, wenye kujitoa kwa ajili yangu na wenye kutaka kabisa kuazibu ubaya. Mumeonyesha katika njia zote kwamba hamukukuwa na kosa katika mambo haya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 7:11
54 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nikawakaripia na kuwalaani, hata nikawapiga wamoja kati yao na kuwaongoa nywele zao. Nikawalazimisha kuapa kwa jina la Mungu, nikisema: “Wabinti zenu musiwaoeshe kwa vijana wao, wala wabinti zao wasiolewe na vijana wenu au na ninyi wenyewe.


Kwa hiyo ninatubu na kujihukumu; ninajinyenyekeza na kuikaa juu ya mavumbi na majivu.


Upendo wangu kwako unanifanya niwake hasira, maana waadui zangu hawajali maneno yako.


Ninamungojea Yawe kuliko vile wazamu wanavyongojea mapambazuko, ndiyo, kuliko vile wazamu wanavyongojea mapambazuko.


Anajibia mahitaji yao wote wanaomwabudu; anasikia kilio chao na kuwaokoa.


Mumutumikie Yawe kwa woga; muiname mbele ya mwana wake na kutetemeka, kusudi asikasirike, nanyi musiangamie kwa rafla; kwa maana hasira yake inawaka haraka. Heri wote wanaokimbilia kwake!


Lakini wao walipokuwa wagonjwa, mimi nilivaa magunia kuonyesha huzuni, nilijitesa kwa kufunga kula chakula. Niliomba nikikuwa nimeinamisha kichwa.


Nimeregea na kupondekanapondekana; ninaugua kwa kusongwa katika moyo.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Wakora.


Nimekuwa mugeni kwa wandugu zangu, kaka na dada zangu hawanitambui.


Mwenye hekima ni mwangalifu na anaepuka uovu, lakini mupumbafu hajizuizi wala hana uangalifu.


Heri mutu anayemwogopa Yawe siku zote, lakini mwenye moyo mugumu atapata hasara.


Unipige kama muhuri ndani ya moyo wako, kama muhuri katika mikono yako. Maana mapendo yana nguvu kama kifo, nao wivu ni mukali kama kaburi. Kuwaka kwake ni kama kuwaka kwa moto, unawaka kama ulimi wa moto.


Katika njia ya maamuzi yako tunakungojea ee Yawe; tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wakamwambia mufalme: Yule Danieli anayekuwa mumoja wa wafungwa kutoka inchi ya Yuda hakuheshimu wewe mufalme wala amri uliyotia sahihi. Anafanya maombi yake mara tatu kila siku.


Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.


Wanafunzi wake wakakumbuka maneno haya yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Upendo wangu kwa ajili ya nyumba yako unanichoma.”


Paulo alipokuwa akingojea Sila na Timoteo kule Atene, moyo wake ukavunjika sana kuona namna muji ule ulivyojaa sanamu za miungu.


Unasema ukweli. Yamekatwa kwa sababu yalikataa kuamini na wewe unasimama imara katika imani yako. Sasa usijivune, lakini uogope!


Na yeyote anayemutumikia Kristo kwa njia hiyo anamupendeza Mungu, naye anapata kuwa mwenye kustahili mbele ya watu.


Lakini ikiwa kwa njia ya ubaya tunaofanya, Mungu anaonekana kuwa mwenye haki, basi tutasema kama Mungu hana haki wakati anapotuazibu? (Ninasema kwa mafikiri ya kimutu.)


kusudi kusikuwe mabishano katikati ya viungo vya mwili, lakini vyote visaidiane sawasawa.


Nanyi munajaa na kiburi. Ninyi mungepaswa kuhuzunika na mutu yule aliyefanya kile kitendo, naye angepaswa kutengwa toka katikati yenu.


Nasi tunaomba Mungu kusudi musifanye jambo lolote baya, nasi hatutaki kuonyesha kwamba tumeshinda. Lakini tunataka mutende mema hata ikionekana kuwa sisi tunashindwa.


Azabu mutu yule aliyopewa na watu wengi kati yenu inatosha kwake.


Lakini tunaonyesha katika mambo yote kwamba sisi ni watumishi wa Mungu: tumedumu sana katika mateso, katika ukosefu na katika taabu.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Nasi hatukufarijiwa kwa kuja kwake tu, lakini vilevile kwa namna ile mulivyomufariji. Tito ametuelezea jinsi munavyokuwa na hamu kubwa ya kuniona, jinsi munavyohuzunika na jinsi munavyojitoa kwa ajili yangu. Kwa hivi sasa ninafurahi zaidi.


Sasa ninafurahi, si kwa sababu muliweza kuhuzunika, lakini kwa sababu huzuni yenu imewawezesha kugeuka toka katika zambi. Kwa maana mumehuzunishwa kufuatana na mupango wa Mungu. Kwa hivi hatukuwatendea ubaya wowote.


Kwa maana ninajua nia yenu nzuri ya kusaidia, nami ninajivuna kwa ajili yenu mbele ya watu wa Makedonia, nikisema: “Kanisa la jimbo la Akaya liko tayari kusaidia tangia mwaka jana.” Hivi kwa njia ya bidii yenu mumewavuta wengi kati yao kwa kutoa vilevile.


Kama mukikasirika, musianguke katika zambi, kasirani yenu isidumu muchana kutwa,


Musishiriki katika matendo ya giza yasiyofaa, lakini muyafichue.


Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


Wale wenye kufanya zambi, uwakaripie mbele ya watu kusudi wengine wapate kuogopa vilevile.


Ufanye juhudi kusudi upate kuhesabiwa mbele ya Mungu kama mutu anayemupendeza, ukiwa kama mutumishi asiyesikia haya juu ya kazi yake, lakini anayetangaza kwa haki ujumbe wa kweli wa Mungu.


Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.


Basi kwa kuwa tungali na ahadi ya kuingia kwenye mapumziko yale, basi tufanye angalisho kusudi katikati yenu kusikuwe hata mutu mumoja atakayekosa kuingia.


Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.


Na ikiwa katika maombi yenu munamwita “Baba” yule anayehukumu kila mutu pasipo upendeleo kufuatana na matendo yake, basi muishi katika heshima mbele yake kwa muda unaowabakilia kwa kuishi hapa katika dunia.


Kama vile watoto wachanga wanaotamani maziwa, na ninyi vilevile mukuwe na hamu ya kunywa maziwa safi ya kiroho, kusudi mupate kukomaa na kuokolewa.


muwaokoe, mukiwaopoa toka katika moto. Muwasikilie vilevile wengine huruma, lakini kwa woga, mukichukia hata nguo zao zilizochafuliwa na tamaa zao mbaya.


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ