Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 6:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 kama watu wasiojulikana ingawa tunajulikana vizuri, kama wanaokufa ingawa sisi ni wazima. Tunaazibiwa lakini hatuuawi,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 6:9
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walimu wamoja wa kikundi cha Waepikurio na cha Wastoiko, wakaanza kubishana na Paulo. Wamoja wao wakauliza: “Huyu katetea anataka kusema nini?” Wengine wakasema: “Anaonekana kuwa muhubiri wa miungu ya kigeni.” Walisema hivi kwa sababu Paulo alikuwa akihubiri juu ya Yesu na jinsi alivyofufuka.


Sasa ninyi wenyewe munaona na kusikia namna huyu Paulo anayofanya. Amekwisha kuwavuta na kuwaonya watu wengi, si hapa Efeso tu, lakini ni karibu katika jimbo lote la Azia. Anasema kwamba miungu inayotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.


Walikuwa tu wakibishana naye juu ya dini yao wenyewe na juu ya mutu mumoja aliyeitwa Yesu; lakini Paulo alidai kwamba yuko muzima.


Mimi sina maneno kamili ya kumwandikia Mufalme wa Roma juu yake. Ndiyo maana nimemuleta mbele yenu na zaidi mbele yako, wewe mufalme Agripa, kusudi kisha kumwuliza, nipate maneno ya kuandika.


kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kwa sababu yako tunauawa kila siku. Tunahesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”


Lakini tunahukumiwa na kuazibiwa na Bwana kusudi tusiazibiwe pamoja na watu wa dunia hii.


Wandugu zangu, kila siku ninapatwa na hatari ya kufa. Na hii ni hakika sawa vile ninavyojivuna kwa ajili yenu katika kuungana kwangu na Yesu Kristo Bwana wetu.


Kwa maana inaonekana kuwa Mungu ametufanya sisi mitume kuwa watu wenye hali ya chini kabisa. Tunahesabiwa kama watu wanaohukumiwa kufa mbele ya watu. Tumewekwa kama kitu cha kushangaza, kinachoangaliwa na dunia nzima, nao wamalaika na watu vilevile.


Inaonekana kuwa mimi si mutu anayeelewa kusema, lakini kwa ngambo ya elimu, mimi ninaielewa sana. Nasi tumeonyesha hayo yote kila wakati na katika mambo yote.


Tumekataa mambo ya kisirisiri na ya haya. Hatuna mwenendo wa udanganyifu wala hatupotowi neno la Mungu. Lakini tunajulisha waziwazi ukweli kusudi tuvute kila mutu kutuaminia katika zamiri yake mbele ya Mungu.


Basi, kwa sababu tunajua kwamba ni lazima kumwogopa Bwana, ndiyo maana tunajitoa kuwavuta watu kwake. Mungu anatujua waziwazi nami ninatumaini kwamba ninyi wenyewe munatujua waziwazi vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ