Alivaa haki kama vile nguo ya kujikinga kifua, na wokovu kama kofia ya chuma juu ya kichwa. Alivaa nguo ya kulipiza kisasi, na kujifunika na kanzu ya wivu.
Ni kweli Kristo alitundikwa juu ya musalaba katika hali ya uzaifu wa mwili, lakini sasa anaishi kwa uwezo wa Mungu. Nasi katika kuungana kwetu naye sisi vilevile tunakuwa zaifu. Lakini kwa ajili yenu tunaishi pamoja naye kwa nguvu ya Mungu.
Basi sisi si kama wengine wengi wanaochuuza neno la Mungu; lakini kwa sababu Mungu ndiye aliyetutuma, sisi tunasema ukweli mbele yake, kama vile watumishi wa Kristo.
Tumekataa mambo ya kisirisiri na ya haya. Hatuna mwenendo wa udanganyifu wala hatupotowi neno la Mungu. Lakini tunajulisha waziwazi ukweli kusudi tuvute kila mutu kutuaminia katika zamiri yake mbele ya Mungu.
Mimi nimejivuna kidogo mbele yake kwa ajili yenu, nami sikupata haya. Lakini kama vile tulikuwa tunawaambia kila mara ukweli, vilevile kule kujisifu kwetu kwa ajili yenu mbele ya Tito, kumeonekana kuwa kwa kweli.
Ninyi vilevile, wakati muliposikia ujumbe wa kweli, maana yake Habari Njema iliyowaletea wokovu, mukamwamini Kristo. Naye Mungu akawapatia Roho Mutakatifu aliyeahidi kuwa kitambulisho cha kuhakikisha kwamba ninyi ni watu wake kabisa.
Imani yenu na upendo wenu vinakuwa na musingi katika tumaini mulilowekewa mbinguni. Mulisikia juu ya tumaini lile mara ya kwanza wakati mulipohubiriwa ujumbe wa ukweli ni kusema Habari Njema.
Lakini sisi ni watu wa muchana, tunapaswa kuwa wakadirifu. Tunapaswa kushikamana na imani na upendo kama vile nguo ya chuma ya kukingia kifua, nalo tumaini letu la wokovu kama vile kofia ya kutulinda.
Ufanye juhudi kusudi upate kuhesabiwa mbele ya Mungu kama mutu anayemupendeza, ukiwa kama mutumishi asiyesikia haya juu ya kazi yake, lakini anayetangaza kwa haki ujumbe wa kweli wa Mungu.
Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.