Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Sisi hatutaki kumukwaza mutu yeyote katika jambo lolote kusudi kazi yetu isizarauliwe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 6:3
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini haifai kuwakwaza. Kwa hiyo kwenda kwenye ziwa, na utupe ndoana ndani ya maji. Na samaki wa kwanza utakayemunasa, ufungue kinywa chake, nawe utaona kikoroti cha feza. Ukikamate na kukitoa kwa kulipa kodi kwa ajili yetu sisi wawili.”


“Lakini anayeangusha mumoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingalikuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kuzamishwa ndani ya bahari.


Hivi kunakuwa hatari, na si kwa kazi hii yetu kuzarauliwa tu, lakini vilevile hekalu la mungu mukubwa muke, Artemi, litahesabiwa kuwa kitu bure. Na tena utukufu wake utapunguka, yeye anayeabudiwa na watu wote wa Azia na dunia nzima!”


Basi tusihukumiane tena sisi wenyewe. Lakini tafazali mukamate kusudi hili: mutu asifanye kitu kinachoweza kumukwaza au kumwangusha ndugu yake katika zambi.


Ikiwa wengine wako na haki ya kupata vitu kama vile toka kwenu, sisi hatuna haki zaidi kuliko wao? Sisi hatudai kutendewa sawa na haki yetu, lakini tunavumilia kusudi tusiiwekee Habari Njema ya Kristo kizuizo chochote.


Na kwa wale wanaokuwa zaifu katika imani, ninajifanya kama muzaifu kusudi niwapate hao wanaokuwa zaifu. Kwa wote nimejifunza kuwa mwenye hali kama yao, kusudi nipate kuokoa wamoja kati yao kwa njia mbalimbali.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Tunaepuka kushitakiwa na watu wengine juu ya mali mingi kama hii tunayochunga.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ