Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 5:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Lakini mbele ya yote tunataka sana kumupendeza Bwana, ikiwa tunakaa au kutoka katika mwili huu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 5:9
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ukitenda vyema hautakubaliwa? Na usipotenda vyema, basi, zambi inajificha kwa mulango; inakutamani, lakini unapaswa kuishinda.”


hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi; sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu. Maana nyumba yangu itaitwa: Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.


Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”


lakini katika kila taifa mutu yeyote anayemutii Mungu na kutenda yanayokuwa ya haki, anamupendeza.


Na yeyote anayemutumikia Kristo kwa njia hiyo anamupendeza Mungu, naye anapata kuwa mwenye kustahili mbele ya watu.


Maana kama tunaishi, tunaishi kwa ajili ya Bwana, na kama tunakufa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi ikiwa tunaishi, au ikiwa tunakufa, sisi ni watu wa Bwana.


Nayo nia moja niliyokuwa nayo ni kuhubiri tu Habari Njema fasi zote ambapo habari za Kristo zilipokuwa hazijasikilika bado. Nilikusudia vile kusudi nisijenge juu ya musingi uliowekwa na mutu mwingine,


Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.


Basi tuna uhodari siku zote. Tunajua kwamba wakati tunapoishi katika mwili huu, tunaishi mbali na makao ya Bwana.


Sisi tuna uhodari na tungependa zaidi kutoka katika mwili huu na kwenda kuishi pamoja na Bwana.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.


Ni kwa sababu hiyo ninatumika na kupigana kwa uwezo ninaopewa na Kristo, unaoniwezesha kufanya kazi kwa nguvu.


Kwa mwisho, wandugu, sisi tumewafundisha namna gani munavyopaswa kuishi kusudi mupate kumupendeza Mungu. Na kweli, ni vile munavyoishi. Na sasa, tunawaomba na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu, muendelee mbele vizuri zaidi katika mwenendo ule.


Mufanye bidii sana mupate kuishi katika amani. Mushugulike na mambo yenu ninyi wenyewe na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe sawa vile tulivyokwisha kuwaagiza.


Na ni kwa hiyo tunasumbuka na kupigana, kwa maana tunamutumainia Mungu Mwenye Uzima, Mwokozi wa watu wote na hasa zaidi Mwokozi wa waamini.


Basi kwa kuwa tunakubaliwa kuwa washiriki wa ufalme usioweza kutikiswa, tukuwe watu wenye shukrani. Tuonyeshe shukrani ile kwa kumwabudu Mungu kwa njia inayomupendeza kwa heshima na woga,


Basi tufanye bidii ya kuingia kwenye mapumziko yale, kusudi hata mutu mumoja asianguke sawa vile wale walioasi katika jangwa.


Kwa sababu hiyo, wapendwa wangu, mukiwa munangojea mambo yale, mufanye bidii apate kuwakuta safi bila kosa lolote na mukae na amani pamoja naye.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ