Basi, Musa alipoona kwamba watu wameasi na kufanya wanavyopenda (kwa kuwa Haruni aliwafanya waasi na kufanya wanavyopenda na kujiletea haya mbele ya waadui zao),
Hakika kwa wakati wowote tungali tunaishi katika makao haya ya dunia, tunaugua kwa kulemewa. Si kwa sababu tunataka kuondolewa mwili wa dunia, lakini tunataka kuvaa mwili wa mbinguni, kusudi uzima wa milele upate kubadilisha miili yetu inayokuwa ya kufa.
“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”
Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.