Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 4:4
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwuliza: ‘Kwa namna gani?’ Naye akajibu: ‘Nitakwenda na kuwasukuma manabii wake wote waseme uongo.’ Yawe akamwambia: ‘Wewe utamushawishi na utashinda; basi, kwenda ufanye hivyo.’


Kutoka Sayuni, muji muzuri kupita kipimo, Mungu anajitokeza, akiangaza.


Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika miiba, ni mufano wa wale wanaosikia Neno la Mungu, lakini masumbuko ya dunia hii na udanganyifu wa mali vinasonga lile neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


Sasa ni wakati wa dunia hii kuhukumiwa; sasa mutawala wa dunia hii atashindwa.


Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.


“Mungu amepofusha macho yao, kusudi yasipate kuona. Ameifanya mioyo yao kuwa migumu, wala wasipate kunigeukia nami ningewaponyesha.”


Anayeniona amemwona vilevile yule aliyenituma.


Sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa sababu mutawala wa dunia hii anakuja. Yeye hana uwezo juu yangu,


Kama nisingetenda kati yao matendo yasiyofanywa na mutu mwingine, wasingekuwa na zambi. Lakini sasa wameyaona lakini hata hivi wananichukia mimi pamoja na Baba yangu.


Na kuelekea hukumu ni kwa sababu mutawala wa dunia hii amekwisha kuhukumiwa.


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Wao walitangaza kwamba Kristo anapaswa kuteswa na kuwa wa kwanza kufufuka kati ya wote waliokufa, naye atahubiri kwa Wayuda na kwa watu wa mataifa mengine kwamba kwa njia ya kuokolewa wataweza kuishi katika mwangaza.”


Hapana. Ninataka kusema kwamba vitu wapagani wanavyotambikia, wanavitolea pepo wala si Mungu. Nami sipendi mushirikiane na pepo hata mara moja.


kusudi Shetani asipate njia ya kutushinda, maana tunajua nia zake.


Wakati nilipofika katika muji Troa kwa kutangaza Habari Njema ya Kristo, Bwana alinipatia wakati muzuri wa kutumika kule.


Kwa maana kama mambo yaliyokuwa ya muda tu yalipata utukufu, basi yale yanayodumu ni yenye utukufu zaidi.


Lakini akili yao ilikuwa nzito kwa kufahamu. Kwa maana mpaka sasa, Waisraeli wanaposoma katika vitabu vya Agano la Kale, akili yao inafunikwa na kitambaa kile kile. Kitambaa kile kitaondolewa tu kwa mutu anayeungana na Kristo.


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Kristo alijitoa mwenyewe kwa kutuokoa toka katika zambi zetu, kusudi atukomboe katika dunia hii mbaya ya sasa, kwa mapenzi ya Mungu Baba yetu.


Mulikuwa mukiishi kufuatana na mwenendo mubaya wa dunia hii. Mulitii mutawala wa roho zenye uwezo wa anga anayetawala sasa watu wasiomutii Mungu.


Kwa maana hatupigani na watu wa dunia hii, lakini tunapigana na pepo mbaya zinazokaa katika eneo la mbingu pamoja na wakubwa, na wenye mamlaka na watawala wa dunia hii ya giza.


Tangu mwanzo yeye alikuwa na hali ya Mungu, lakini hakuona kwamba kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho.


Kristo ni mufano kamili wa Mungu asiyeonekana. Yeye ni muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.


Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.


Mafundisho haya yanalingana na Habari Njema ya utukufu wa Mungu mwenye baraka, ambayo nilipewa nipate kuihuburi.


Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Maana watu wanapokwisha kuangaziwa na ukweli wa Mungu na kuonja zawadi ya mbinguni, na kuishi katika ushirika na Roho Mutakatifu,


Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.


Lakini anayemuchukia ndugu yake anaishi na kutembea katika giza, wala hajui pahali anapokwenda kwa sababu giza limemupofusha macho.


Kwa ngambo ingine amri hii ninayowaandikia ni mupya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu vilevile. Kwa maana giza linapita na mwangaza wa kweli umekwisha kutokea.


Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ