13 Maandiko Matakatifu yanasema: “Niliamini ndiyo maana nilisema.” Sisi vilevile tunakuwa na imani ile ile, ndiyo maana tunasema.
Nilikuwa na imani hata niliposema: “Mimi nimetaabika sana.”
Mushuhuda mwongo ataangamia, lakini anayejua kusikiliza hawezi kunyamazishwa.
Haipaswi kuwa vile, kwa maana sisi na wao vilevile tunaamini kwamba sisi wote tunaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu.”
Ni kusema kwamba nipate kutiwa moyo kwa njia ya imani yenu na ninyi kwa njia ya imani yangu.
Mwingine anapewa imani na Roho yule yule na mwingine uwezo wa kuponyesha wagonjwa.
Na kwa sababu tunakuwa na tumaini lile, sisi tunasema kwa uhodari.
Kwa hivi, kifo kinafanya kazi ndani yetu, lakini uzima unafanya kazi ndani yenu.
Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.