Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kila wakati tunabeba mateso ya kufa kwa Yesu katika mwili wetu, kusudi uzima wa Yesu uonekane vilevile ndani ya mwili wetu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 4:10
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kunabaki wakati kidogo, dunia haitaniona tena, lakini ninyi mutaniona; na kwa sababu mimi ninaishi, ninyi mutaishi vilevile.


Ikiwa tuliungana naye kwa njia ya kufa kama yeye, tutaungana naye vilevile kwa njia ya kufufuliwa kama yeye.


Ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pamoja naye vilevile.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kwa sababu yako tunauawa kila siku. Tunahesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”


Basi, kwa kadiri tunavyoshiriki katika mateso mengi ya Kristo, ni kwa kadiri ile sisi vilevile tunafarijiwa sana kwa njia ya Kristo.


Tulikuwa tumefikiri kwamba tulihukumiwa kufa. Basi, ilitokea hivi kusudi tusijitegemee sisi wenyewe, lakini tumutegemee Mungu tu anayefufua wafu.


Ni kweli Kristo alitundikwa juu ya musalaba katika hali ya uzaifu wa mwili, lakini sasa anaishi kwa uwezo wa Mungu. Nasi katika kuungana kwetu naye sisi vilevile tunakuwa zaifu. Lakini kwa ajili yenu tunaishi pamoja naye kwa nguvu ya Mungu.


Kwa maana katika maisha yetu, tunakuwa kila mara katika hatari ya kufa kwa ajili ya Yesu, kusudi uzima wake uonekane vilevile katika mwili wetu unaokuwa wa kufa.


Basi sasa, mutu asinisumbue tena kwa maana niko na makovu juu ya mwili wangu niliyopata kwa ajili ya Yesu.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Maneno haya ni ya kuaminiwa: Kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye vilevile.


Lakini mufurahi kwa sababu munashiriki katika mateso ya Kristo. Na kwa hiyo mutashangilia kwa furaha wakati atakapoonekana katika utukufu.


Ninyi ni wenye heri kama watu wakiwatukana kwa ajili ya Kristo, kwa kuwa Roho wa utukufu, maana yake Roho wa Mungu anakaa ndani yenu.


Wakati nilipomwona, nikaanguka chini kwa rafla mbele yake kama vile mufu. Lakini akaweka mukono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ