Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kwa wema wake, Mungu ametupatia utumishi huu, na kwa sababu hii sisi hatukati tumaini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 4:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata vijana wataregea na kuchoka; kweli washujaa wataanguka kwa muchoko.


Lakini wote wanaomutumainia Yawe, watapata nguvu mupya. Watapanda juu kwa mabawa kama tai, watakimbia bila kuchoka, watatembea bila kuregea.


Wewe ulisema: Ole wangu! Yawe ameongezea uchungu juu ya maumivu yangu. Nimechoka na kulalamika, wala siwezi kupumzika.


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu kwa kuwaonyesha kwamba wanapaswa kuomba siku zote pasipo kuchoka.


Basi, Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi wa Mungu, waliowaonyesha ninyi njia ya kuamini. Tumefanya vile kila mumoja wetu kwa kadiri ya zawadi aliyopewa na Bwana.


Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mutu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana.


Na kwa sababu tunakuwa na tumaini lile, sisi tunasema kwa uhodari.


Kwa maana Mungu ndiye aliyetuwezesha kuwa watumishi wa agano jipya, lisilotokana na Sheria iliyoandikwa, lakini na Roho. Sheria iliyoandikwa inaleta kifo lakini Roho analeta uzima.


Kwa sababu hii hatukati tumaini hata kidogo. Ijapokuwa hali yetu ya kimwili inaharibika, hali yetu ya kiroho inafanywa upya siku kwa siku.


Mambo haya yote yalifanyika na Mungu, aliyetupatanisha naye kwa njia ya Kristo na kutupatia kazi ya kuongoza watu wengine wapatane naye.


Tusichoke kutenda mema; kwa maana siku zitakapotimia tutavuna kama tusiporegea.


Basi ninawaomba musiregee kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, kwa maana yanawaletea utukufu.


Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Ingawa zamani nilikuwa mwenye kumutukana, mwenye kumutesa na kumutendea kwa ukali, lakini amenihurumia, kwa sababu yote niliyofanya, niliyafanya kwa upumbafu kwa maana sikukuwa bado na imani.


Kwa hiyo mumukumbuke yule aliyevumilia kutendewa na wenye zambi kwa chuki kubwa, kusudi musipate kuchoka wala kuregea.


Zamani ninyi hamukukuwa watu wa Mungu, lakini sasa munakuwa watu wake; zamani ninyi hamukuhurumiwa na Mungu, lakini sasa mumehurumiwa naye.


Wewe ni muvumilivu; umeteswa kwa ajili ya jina langu, lakini haukuregea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ