Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Sheria ile inayoleta kifo imeandikwa neno kwa neno juu ya vibao vya mawe na utukufu wa Mungu ulingaa wakati ule. Uso wa Musa ukangaa vilevile hata Waisraeli hawakuweza kuangalia uso wake ingawa kungaa kule kulikuwa kwa muda tu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 3:7
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe Mungu akawatengenezea Adamu na muke wake nguo za ngozi, akawavalisha.


Kule kwa mulima Sinai ulishuka toka mbinguni na kuzungumuza nao. Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli, masharti mazuri na amri.


Ninatamani sana uniokoe, ee Yawe; sheria yako ndiyo furaha yangu.


Ninapenda sana sheria yako! Ninafikiri juu yake muchana kutwa!


Yawe akamwambia Musa: Kuja kwangu juu kwenye mulima, ungoje kule. Mimi nitakupa vibao vya mawe vyenye sheria na amri nilizoandika kwa ajili ya kuwafundisha Waisraeli.


Yawe alipomaliza kuongea na Musa juu ya mulima Sinai, akamupatia Musa vile vibao viwili vya mawe ambavyo juu yake Mungu aliziandika zile amri kwa kidole chake mwenyewe.


Mara tu walipokaribia kambi walimwona yule mwana-ngombe na watu wakicheza. Hapo hasira ya Musa ikawaka kama moto, akatupa chini vile vibao kutoka mikono yake na kuvivunja pale chini ya mulima.


Yawe akamwambia Musa: Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika maneno yale yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza ulivyovunja.


Na wote waliohuzuria katika lile Baraza wakamukazia Stefano macho, wakaona uso wake unafanana sawa na uso wa malaika.


Kwa maana kwa njia ya Kristo, Sheria imepata kufikia ukomo wake kusudi kila mutu anayeamini apate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Kwa sababu Sheria inaamusha kasirani ya Mungu. Lakini Sheria haingekuwa, kuvunja Sheria hakungekuwa vilevile.


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


nami nikakufa. Hivi ile amri iliyopasa kuniletea uzima ikaniletea kifo.


Ndani ya roho yangu ninapendezwa na Sheria ya Mungu,


Kwa maana tulipoishi maisha ya kimwili, tamaa ya kufanya zambi iliyotokana na Sheria ilitumika ndani yetu na kutuletea kifo.


Lakini wakati mambo matimilifu yatakapokuja, yale yasiokuwa matimilifu yatatoweka.


Inaonekana wazi kwamba ninyi ni barua iliyoandikwa na Kristo na kutumwa kwa njia ya utumishi wetu. Barua hii inaandikwa si kwa wino, lakini kwa Roho wa Mungu Mwenye Uzima. Barua hiyo haikuandikwa juu ya vibao vya mawe, lakini katika mioyo ya watu.


Kwa maana Mungu ndiye aliyetuwezesha kuwa watumishi wa agano jipya, lisilotokana na Sheria iliyoandikwa, lakini na Roho. Sheria iliyoandikwa inaleta kifo lakini Roho analeta uzima.


Basi si zaidi sana matokeo ya utumishi wa Roho yatakuwa yenye utukufu?


Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”


Basi, ni kusema kwamba Sheria haipatani na ahadi za Mungu? Hapana, hata kidogo! Kama kungetolewa Sheria yenye uwezo wa kuleta uzima kwa watu, basi mutu angehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria.


Naye akawatangazia agano lake akawaamuru mulishike maana yake mutii zile amri kumi ambazo aliandika juu ya vibao viwili vya mawe.


Wala hakuna taifa lingine lolote hata likuwe kubwa namna gani, lenye masharti na maagizo ya haki, kama hayo ambayo nimewafundisha siku hii ya leo.


“Hizi ndizo amri Yawe alizowaambia ninyi wote kwa sauti kubwa kutoka katika moto na lile wingu zito na giza nene, mulipokuwa mumekusanyika kule kwenye mulima. Hakuongeza hapo amri ingine. Kisha akaandika juu ya vibao viwili vya mawe, akanipatia.


“Basi, nikageuka, nikashuka kutoka kwenye mulima, nikiwa nimebeba vile vibao viwili vya agano, nao moto ulikuwa unawaka juu ya mulima.


Ninyi hamujafikia kwenye kitu kinachoweza kuguswa kama vile Waisraeli walivyofikia kwenye mulima Sinai. Mulima ule uliwaka moto, ulifunikwa na giza nzito, nao ulikuwa na uvumi wa zoruba juu yake.


Mujengaji wa nyumba anaheshimiwa zaidi kuliko nyumba yenyewe. Hivi vilevile Yesu anastahili kupewa heshima kubwa zaidi kuliko Musa.


Ndani ya chumba kile kulikuwa chombo cha kufukizia ubani, kilichotengenezwa na zahabu. Na kulikuwa vilevile Sanduku la Agano lililopakaliwa zahabu pande zote. Ndani ya sanduku lile kulikuwa kopo la zahabu lenye mana, na fimbo ya Haruni iliyoota vichipukizi juu yake. Kulikuwa vilevile vibao vya mawe vyenye Maandiko ya Agano la Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ