Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 3:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Na kwa sababu tunakuwa na tumaini lile, sisi tunasema kwa uhodari.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 3:12
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Wayuda wakamuzunguka, na kumwambia: “Mpaka wakati gani utatuzungusha kichwa? Kama wewe ni Kristo, utuambie waziwazi.”


“Nimewaambia ninyi maneno hayo kwa mifano. Lakini kutakuwa wakati sitasema nanyi tena kwa mifano, lakini nitawaambia ninyi waziwazi juu ya Baba.


Basi wanafunzi wake wakamwambia: “Sasa unasema waziwazi pasipo kutumia mifano.


Paulo na Barnaba wakakaa Ikonio kwa muda murefu. Walisema kwa uhodari kabisa, wakimutumainia Bwana. Naye aliwapa uwezo wa kufanya maajabu na vitambulisho. Na kwa njia hiyo alihakikisha kwamba ujumbe walioutangaza juu ya neema yake ulikuwa wa kweli.


Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Basi Barnaba akamutwaa na kumupeleka kwa mitume. Akawaelezea namna Saulo alivyomwona Bwana katika njia na jinsi Bwana alivyosema naye. Akawaelezea vilevile namna Saulo alihubiri kwa jina la Yesu pasipo woga katika Damasiki.


Vilevile alisemezana na kubishana na Wayuda waliosema kigriki, lakini wao walitafuta njia ya kumwua.


Lakini, katika mukutano ninapenda kusema maneno matano yenye kusikilika, kusudi niwafundishe wengine, kuliko kusema maneno elfu kumi kwa luga za ajabu.


Sasa mimi Paulo mwenyewe ninawaomba kwa upole na kwa wema sawa na ule wa Kristo; mimi yule ambaye wanasema juu yake kwamba ni mupole wakati ninapokuwa pamoja nanyi, lakini ni mukali wakati ninapokuwa mbali nanyi.


Kwa maana kama mambo yaliyokuwa ya muda tu yalipata utukufu, basi yale yanayodumu ni yenye utukufu zaidi.


Maandiko Matakatifu yanasema: “Niliamini ndiyo maana nilisema.” Sisi vilevile tunakuwa na imani ile ile, ndiyo maana tunasema.


Mimi ninawaaminia sana na kujivuna kwa ajili yenu. Katika mateso yetu yote, ninafarijiwa sana na kujazwa na furaha.


Kwa ajili ya kufungwa kwangu, wandugu wengi wamemwamini Bwana na kuwa na bidii sana ya kutangaza Neno la Mungu pasipo woga.


Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.


Basi muniombee kusudi nipate kuupasha waziwazi sawa ninavyopaswa kufanya.


Kama vile munavyojua, mbele ya kufika kwenu tuliteswa na kutukaniwa kwanza katika muji Filipi. Lakini ingawa tulipata vizuizo vingi, Mungu alitupatia uhodari wa kuwapasha ninyi Habari yake Njema.


Wasaidizi wanaotumika vizuri kazi zao, wanajiheshimisha, na wanaweza kutangaza kwa uhodari habari za imani tunayokuwa nayo katika kuungana na Kristo Yesu.


Kwa sababu hii, ingawa ninakuwa na mamlaka niliyopewa na Kristo kukuagiza neno unalopaswa kufanya,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ