8 Kwa hiyo ninawasihi ninyi kuhakikisha upendo wenu kwa mutu yule.
Basi sasa ni afazali kumusamehe na kumufariji, na kuepuka asikate kitumaini kwa sababu ya huzuni kubwa.
Kwa maana shabaha yangu ya kuwaandikia ile barua ni kutaka kuwapima nipate kujua kwamba muko tayari kunitii siku zote.
Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.
Basi, tunapokuwa bado na wakati, tufanye mema kwa watu wote, na zaidi kwa wandugu zetu katika imani.