Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ni kwa sababu hii niliwaandikia kwamba sitakuja tena kwenu nisihuzunishwe na watu waliopaswa kunifurahisha. Maana nina uhakika kwamba mimi ninapofurahi, ninyi wote munafurahi vilevile.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 2:3
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi munataka nini? Nifike kule kwenu, nikikuja na fimbo au na moyo unaojaa upendo na upole?


Katika tumaini hili nilikusudia kufika kwenu kwanza kusudi mupate furaha mara mbili.


Ninamutaja Mungu kuwa mushuhuda wangu, yeye anajua roho yangu! Mimi nilikusudia kutorudia tena Korinto kwa sababu ya kuwasikilia huruma.


Ninasema kama mupumbafu, lakini ni ninyi ndio mumenilazimisha kufanya vile. Kufuatana na ile, ningepaswa kusifiwa nanyi. Kwa maana hata kama mimi si kitu, wale mitume wenu wanaohesabiwa kuwa wakubwa hawanipiti kitu kabisa.


Ninaogopa kwamba kwa safari yangu ingine, Mungu wangu atanifanya tena kuwa mwenye haya mbele yenu. Nami nitalia kwa ajili ya watu wengi waliofanya zambi zamani nao hawakugeuka toka katika uasherati, uzinzi na tamaa mbaya walizofanya.


Ni kwa hiyo ninawaandikia maneno haya nikiwa mbali nanyi, kusudi wakati nitakapokuwa kati yenu nisitende kwa ukali kadiri ya mamlaka Bwana aliyonipa. Kwa maana uwezo ule ni kwa ajili ya kuwajenga katika imani, lakini si wa kubomoa.


Kwa maana shabaha yangu ya kuwaandikia ile barua ni kutaka kuwapima nipate kujua kwamba muko tayari kunitii siku zote.


Basi ikiwa nimewaandikia, si kwa ajili ya yule aliyefanya kosa au si kwa ajili ya yule aliyemukosea. Lakini kusudi mupate kutambua waziwazi mbele ya Mungu bidii munayokuwa nayo kwa ajili yetu.


Ninafurahi sana kwa sababu ninaweza kuwaaminia katika kila jambo.


Lakini Mungu anayefariji watu wanyenyekevu, ametufariji kwa njia ya kufika kwa Tito.


Basi, ikiwa nimewahuzunisha na barua yangu, sijuti juu yake sasa. Nilijuta wakati nilipotambua kwamba barua ile iliwahuzunisha ingawa ilikuwa ni kwa muda tu.


Tunatuma ndugu yetu mwingine pamoja nao. Sisi tumemupima mara nyingi na ameonyesha siku zote kwamba yeye ni mwenye bidii sana. Na sasa, yeye ni mwenye bidii zaidi tena kwa kuwa anawaaminia ninyi sana.


Ingawa vile mimi niko na tumaini juu yenu kutoka kwa Bwana kwamba hamutakuwa na nia mbalimbali na mimi. Lakini yule anayewavuruga ataazibiwa hata ikiwa ni nani.


Bwana anatupatia tumaini kwa ajili yenu kwamba munafanya na mutaendelea kufanya yale tunayowaagiza.


Ninapokuandikia, nina uhakika kwamba utanisikia na hata utafanya zaidi kuliko vile nilivyosema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ