Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 2:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini Mungu ashukuriwe, maana yeye ndiye anayetupatia ushindi siku zote katika ushirika wetu pamoja na Kristo. Anatutumia sisi kwa kutambulisha Kristo pahali pote kama vile harufu nzuri ya marasi inavyosambaa popote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 2:14
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utuokoe, ee Yawe, Mungu wetu, utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa, tupate kusifu jina lako takatifu, na kuona utukufu juu ya sifa zako.


Amewapa watu wake nguvu; nayo heshima kwa watu wote waaminifu, ndio watu wa Israeli wapendwa wake. Haleluia!


Manukato yako yananuka vizuri, na jina lako ni kama marasi yenye harufu nzuri. Kwa hiyo wabinti wote wanakupenda!


Kisha kuwatoa toka katika inchi ambako mumesambazwa na kuwakusanya pamoja, nitazipokea sadaka zenu zenye harufu nzuri. Nami nitaonyesha utakatifu wangu kati yenu mbele ya mataifa mengine.


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Kwanza ninamushukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu habari za imani yenu zinasambaa katika dunia nzima.


kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.


Lakini asante kwa Mungu, kwa maana ninyi muliokuwa zamani watumwa wa zambi mumetii sasa kwa moyo wenu wote kanuni za mafundisho muliyopewa.


Lakini katika mambo haya yote tunapata ushindi kabisa kwa njia ya yule aliyetupenda.


Basi mutu mumoja anapewa na Roho uwezo wa kusema maneno ya hekima, na mwingine uwezo wa kusema maneno ya ufahamu na Roho yule yule.


Kile unachopanda si mumea muzima utakaopaswa kutokea nyuma, lakini ni punje tu, labda ya ngano au mbegu ingine fulani.


Lakini tumushukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.


nanyi wenyewe mutatusaidia kwa njia ya maombi. Kwa hivi Mungu atajibu kwa maombi yaliyotolewa na watu wengi kwa ajili yetu na kututendea wema, na watu wengi watamushukuru kwa ajili yetu.


Shukrani kwa Mungu aliyemutia Tito bidii ya kuwasaidia kama vile sisi tunavyokuwa nayo!


Shukrani kwa Mungu kwa ajili ya zawadi yake inayopita kipimo!


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


Mumushukuru Mungu Baba siku zote kwa kila jambo, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.


Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.


Lakini, inawapasa ninyi kuendelea na musingi imara katika imani, musitikiswe na kupoteza lile tumaini mulilopata wakati muliposikia Habari Njema. Mimi Paulo nimewekwa kuwa mutumishi wa kuhubiri Habari Njema ile iliyokwisha kutangazwa kwa watu wote katika dunia.


Habari Njema ile inatoa matunda na kuenea katika dunia yote sawa vile ilivyofanya kwenu tangu siku ile muliposikia wakisema juu ya neema ya Mungu na kupata kuitambua inavyokuwa kweli.


Mungu alinyanganya uwezo wa wakubwa na wenye mamlaka, naye akawaonyesha waziwazi, akiwatembeza kama wafungwa katika maandamano ya ushindi wa Mwana wake.


Kwa maana tokea kwenu neno la Bwana lilienea, si katika Makedonia na Akaya tu, lakini habari za imani kwa Mungu zilisambaa fasi zote, hata sisi hatukukuwa tena na lazima ya kusema neno juu ya ile.


Sijui namna gani tunavyoweza kumushukuru Mungu kwa ajili yenu kwa sababu ya furaha yote tunayokuwa nayo mbele yake kwa ajili yenu.


Basi, ninataka watu waombe Mungu wakiinua mikono juu, ikiwa imetakaswa, nao wafanye vile bila kasirani wala ubishi.


Wewe umesikia mafundisho niliyotoa mbele ya washuhuda wengi. Nawe sasa uyafundishe kwa watu waaminifu watakaoweza vilevile kuyatoa kwa watu wengine.


wakisema: “Amina! Utukufu, sifa, hekima, shukrani, heshima, uwezo, na nguvu ni vya Mungu wetu, milele na milele! Amina!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ