Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Tunafurahi wakati ninyi munapokuwa na nguvu, hata ikiwa sisi ni zaifu. Nasi tunawaombea kusudi mupate kuwa wakamilifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 13:9
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini kila mumoja wetu anapaswa kumupendeza mwingine kwa kumutendea mema na kuweza hivi kumujenga katika imani.


Wandugu zangu, ninawasihi ninyi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mukuwe na masikilizano kusudi matengano yasikuwe katikati yenu. Muishi katika umoja kabisa mukiwa na nia moja na wazo moja.


Sababu ya hii nilikuwa kwenu katika hali ya uzaifu na woga, mwenye kutetemeka sana.


Sisi ni wapumbafu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika kuungana kwenu na Kristo. Sisi ni zaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu. Tunazarauliwa, lakini ninyi munaheshimiwa!


Kama ikinipasa kujivuna nitajivuna kwa ajili ya uzaifu wangu.


Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.


Ni kweli Kristo alitundikwa juu ya musalaba katika hali ya uzaifu wa mwili, lakini sasa anaishi kwa uwezo wa Mungu. Nasi katika kuungana kwetu naye sisi vilevile tunakuwa zaifu. Lakini kwa ajili yenu tunaishi pamoja naye kwa nguvu ya Mungu.


Kwa hivi, kifo kinafanya kazi ndani yetu, lakini uzima unafanya kazi ndani yenu.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Ni kwa hiyo tunamutangaza Kristo kwa watu wote. Tunaonya na kufundisha kila mutu kwa hekima yote, kusudi tuwasaidie watu wote wapate kufikia kuwa wakamilifu katika kuungana kwao na Kristo.


Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.


Usiku na muchana tunamwomba Mungu kwa bidii sana kusudi atupatie njia ya kuweza kuwaona tena na kuwaongezea kile munachokosewa katika imani yenu.


kusudi mutu wa Mungu apate kukamilika na kuwa tayari kabisa kwa kutenda kila kazi njema.


Lakini ninyi mumefikia kwenye mukutano wa furaha wa wazaliwa wa kwanza wa Mungu walioandikwa majina zao katika mbingu. Mumefikia vilevile karibu na Mungu, anayekuwa mwamuzi wa watu wote na kwenye nafsi kunapokuwa roho za watu wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.


awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.


Basi kwa sababu hii, tuache mafundisho ya mwanzo juu ya Kristo. Tusijenge tena musingi mupya wa mambo haya: kugeuka toka katika matendo yasiyofaa, kumwamini Mungu, namna mbalimbali za ubatizo, kuwawekea watu mikono, ufufuko na hukumu ya milele. Tuendelee katika mafundisho makamilifu. Tutafanya hivi, Mungu akitaka.


Lakini mukisha kuteswa kwa muda kidogo, Mungu mwenye neema yote aliyewaita kusudi mupate kushiriki naye katika utukufu wake wa milele katika kuungana kwenu na Kristo, yeye mwenyewe atawakamilisha. Atawatia nguvu na kuwasimamisha imara kabisa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ