2 Wakorinto 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Nitafanya vile kwa sababu ninyi munataka uhakikisho kwamba Kristo anasema kwa njia yangu. Kwenu Kristo si zaifu, lakini anaonyesha uwezo wake kati yenu.
Sasa mimi Paulo mwenyewe ninawaomba kwa upole na kwa wema sawa na ule wa Kristo; mimi yule ambaye wanasema juu yake kwamba ni mupole wakati ninapokuwa pamoja nanyi, lakini ni mukali wakati ninapokuwa mbali nanyi.
Wakati munaposamehe mutu, nami ninamusamehe vilevile. Kwa maana kama ninasamehe, na ikiwa kweli ninakuwa na neno lolote la kusamehe, ninasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
Na Mungu anaweza kuwajalia mema ya kila namna, kusudi siku zote mupate vyote munavyohitaji, na hivi mupate kuzidi kutoshelewa katika kutenda kazi njema.