Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 12:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kama ningetaka kujivuna, singekuwa mupumbafu, maana ningesema tu ukweli. Lakini ninaepuka kujivuna, kusudi watu wasinihesabu kuwa mukubwa kuliko vile wanavyoona nikifanya au kunisikia nikisema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 12:6
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nani basi, anayeweza kuhakikisha kwamba mimi ni mwongo na kuonyesha kwamba maneno yangu si kweli?


Ninasema ukweli kwa kuungana na Kristo. Na kwa uongozi wa Roho Mutakatifu zamiri yangu inanihakikishia kwamba sisemi uongo:


Basi, Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi wa Mungu, waliowaonyesha ninyi njia ya kuamini. Tumefanya vile kila mumoja wetu kwa kadiri ya zawadi aliyopewa na Bwana.


Kama vile Mungu anavyokuwa mwaminifu, hakika mambo tuliyowaambia hayakukuwa ya kusema “Ndiyo” na “Hapana” kwa mara moja.


Mimi ninasema tena: mutu asinizanie kuwa mupumbafu. Kama si vile, basi munihesabu kama mupumbafu, kusudi nami nipate kujivuna kidogo vilevile.


Mungu Baba ya Bwana Yesu, anayetukuzwa hata milele, anajua kwamba sisemi uongo.


Ninasema kama mupumbafu, lakini ni ninyi ndio mumenilazimisha kufanya vile. Kufuatana na ile, ningepaswa kusifiwa nanyi. Kwa maana hata kama mimi si kitu, wale mitume wenu wanaohesabiwa kuwa wakubwa hawanipiti kitu kabisa.


Lakini, kusudi nisijivune kupita kipimo kwa ajili ya kupokea ufunuo wa ajabu, nilitiwa katika mwili wangu kitu kinachoniumiza kama mwiba. Kitu kile ni kama mujumbe wa Shetani kwa kunipiga na kunizuiza nisijivune kupita kipimo.


Ikiwa kweli tunaonekana kuwa wenda-wazimu, ni kwa ajili ya Mungu, lakini kama sisi ni wenye akili sawa, ni kwa faida yenu.


Mimi nimejivuna kidogo mbele yake kwa ajili yenu, nami sikupata haya. Lakini kama vile tulikuwa tunawaambia kila mara ukweli, vilevile kule kujisifu kwetu kwa ajili yenu mbele ya Tito, kumeonekana kuwa kwa kweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ