Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 11:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Lakini ninaogopa kwamba sawa vile nyoka alivyomudanganya Eva kwa werevu wake, mawazo yenu vilevile yasipotoshwe hata mupate kupoteza uaminifu na ukamilifu wenu kwa Kristo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 11:3
47 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyoka alikuwa mwerevu kuliko nyama wote wa pori walioumbwa na Yawe Mungu. Basi, nyoka akamwambia yule mwanamuke: “Ni kweli Mungu alisema musikule matunda ya muti wowote katika bustani?”


Yawe Mungu akamwuliza yule mwanamuke: “Umefanya nini wewe?” Mwanamuke akamujibu: “Nyoka alinidanganya, nami nikakula.”


Adamu akamupa muke wake jina “Eva”, maana alikuwa mama wa wanadamu wote.


Nyoka akamwambia mwanamuke: “Hamutakufa!


Ninashikwa na hasira kali, ninapoona waovu wakivunja sheria yako.


kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao wataonyesha vitambulisho vikubwa na maajabu, hata ikiwezekana, wawadanganye hata watu waliochaguliwa na Mungu.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Aliyepewa zawadi ya kuonya wengine, awaonye. Aliyepewa zawadi ya kutoa, atoe kwa moyo mweupe. Anayesimamia wengine, awasimamie kwa bidii. Aliyepewa zawadi ya kuhurumia wengine, afanye vile kwa furaha.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Munavumilia hata mutu anayewatia katika utumwa, anayeiba mali zenu, anayewagandamiza, anayewazarau na anayewapiga kofi kwenye uso.


Kukiwa mutu anayepatwa na uzaifu, mimi ninajisikia muzaifu vilevile. Kukiwa mutu anayeanguka katika zambi, ninasikia uchungu.


Basi sisi si kama wengine wengi wanaochuuza neno la Mungu; lakini kwa sababu Mungu ndiye aliyetutuma, sisi tunasema ukweli mbele yake, kama vile watumishi wa Kristo.


Tumekataa mambo ya kisirisiri na ya haya. Hatuna mwenendo wa udanganyifu wala hatupotowi neno la Mungu. Lakini tunajulisha waziwazi ukweli kusudi tuvute kila mutu kutuaminia katika zamiri yake mbele ya Mungu.


Ninashangaa sana kuona namna gani munageuka hivi upesi kwa kumwacha yule aliyewaita kwa njia ya neema ya Kristo na kufuata habari njema ya namna ingine.


ijapokuwa wandugu wamoja wa uongo waliojiunga nasi kwa kisirisiri walitaka kumutahiri. Watu hao walijiingiza katika kikundi kusudi wapate kupeleleza jinsi tunavyoishi katika uhuru kutokana na kuungana kwetu na Yesu Kristo. Walitaka kututia katika maisha ya kitumwa.


Ee ninyi Wagalatia! Ninyi wajinga! Ni nani aliyewaloga? Habari juu ya kutundikwa kwa Yesu Kristo juu ya musalaba ilielezwa waziwazi mbele ya macho yenu.


Ninawaogopea, kwa maana inawezekana kwamba nimesumbuka bure kwa ajili yenu!


Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukipeperushwa na kuvutwa na mafundisho ya kila aina yanayoletwa na watu wanaodanganya wengine na kuwapotosha kwa mayele yao.


Basi munapaswa kutupilia mbali ile hali yenu ya zamani, ule utu wenu wa zamani unaopotoka kufuatana na tamaa zake za udanganyifu.


Ninawatakia neema wale wote wanaomupenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usiokuwa na mwisho.


Musikubali kuhukumiwa na mutu yeyote anayejionyesha kwa inje kuwa yeye ni munyenyekevu na mwenye kuabudu malaika. Mutu wa namna hii anatia sana maana juu ya maono anayopata, naye anajitapa bure juu ya mafikiri yake ya kimutu.


Ninawaambia ninyi maneno haya kusudi mutu asiwadanganye kwa maneno matamu ya kupotosha.


Mujiangalie hata mutu asiwapotoshe kwa elimu yake ya udanganyifu mutupu inayotegemea desturi za watu na roho mbaya zinazotawala dunia, lakini haitegemei mafundisho ya Kristo.


Ni kwa sababu hiyo, nilipoona kwamba siwezi kuendelea kungojea, nilimutuma Timoteo kusudi nipate kujua habari ya imani yenu. Niliogopa kwamba labda yule mushawishi Shetani amejaribu kuwaangusha ninyi na kwamba kazi yote tuliyofanya kwenu imepotea bure.


Ukae kule Efeso sawa vile nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia. Na kule uwazuize wale watu wanaofundisha mafundisho ya uongo.


Na si Adamu aliyedanganywa, lakini ni mwanamuke ndiye aliyedanganywa na kuasi agizo la Mungu.


Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.


Kufuatana na hiyo, kuna watu wengi hasa kati ya Wayuda walioamini, wanaokuwa waasi, wakatetea na wadanganyifu.


Musidanganywe na mafundisho mengine ya kigeni ya kila namna. Kwa maana mioyo yetu inapaswa kutiwa nguvu kwa njia ya neema ya Mungu, wala si kwa njia ya kushika kanuni zinazoagizwa juu ya vyakula. Kanuni hizo haziwafalii kitu wale wanaozishika.


Basi ninyi wapendwa wangu, mumekwisha kutambua mambo haya. Mujiangalie vizuri kusudi musipotoshwe na makosa ya watu waovu na kukosa kusimama imara.


Mbele ya yote, mujue kwamba katika siku za mwisho kutakuja watu watakaoishi kufuatana na tamaa zao wenyewe. Watawachekelea ninyi


Watoto wangu, huu ni wakati wa mwisho. Mulisikia habari kwamba mupinga Kristo atakuja, lakini hata sasa wapinga Kristo wengi wametokea. Na kwa hiyo tunajua kwamba ni wakati wa mwisho.


Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.


Maana kuna watu wasiomuheshimu Mungu waliojiingiza kwa siri kati yetu. Watu hawa wanapotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu kusudi wapate kufanya uasherati na kumukana Yesu Kristo, anayekuwa peke yake Kiongozi na Bwana wetu. Tangia zamani Maandiko Matakatifu yamejulisha hukumu ile itakayowapata watu hawa.


Basi yule nyoka akatokeza maji kwa uwingi ndani ya kinywa chake, nayo yakatelemuka kama muto nyuma ya yule mwanamuke kusudi yapate kumupeleka.


Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.


Akamukamata yule nyoka mukubwa, ndiye yule nyoka wa zamani, anayeitwa “Mwovu” au “Shetani” na kumufunga kwa muda wa miaka elfu moja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ