Alifanya vile kusudi maagizo ya haki ya Sheria yapate kutimizwa ndani yetu sisi tunaoishi kufuatana na uongozi wa Roho wa Mungu, lakini si kufuatana na hali yetu ya kimwili.
Basi, nilipokusudia kubadilisha mupango wangu mimi nimekuwa kama kigeugeu? Wakati ninapofanya mipango yangu, mimi ninaongozwa na mafikiri ya kimutu hata nipate kusema “Ndiyo” na “Hapana” kwa mara moja?
Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.
Timoteo mwana wangu, ninakupa agizo hili kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Maneno hayo ndiyo yatakayokuwezesha kupiga vita nzuri,
Nasi vilevile tunazungukwa na kundi kubwa kama lile la wale walioshuhudia imani yao. Basi tutupilie mbali vitu vyote vinavyotusonga, nazo zambi zinazotufunga upesi na tukimbie kwa juhudi sana katika mashindano tunayowekewa.