Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 10:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa kweli hatungesubutu kujifananisha au kujilinganisha na watu wale wanaojisifu wenyewe. Wao ni wapumbafu. Wanajipima kufuatana na kipimo chao wenyewe na kujilinganisha na wao wenyewe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 10:12
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hakika! Ninyi ni watu wa hekima. Hekima itakufa wakati ule mutakapokufa.


Si vizuri kula asali nyingi sana; vilevile haifai kujipendekeza sana.


Unamwona mutu anayejiona kuwa mwenye hekima? Afazali kumutumainia mupumbafu kuliko yule.


Acha watu wengine wakusifu, kuliko kujisifu kwa mudomo wako wewe mwenyewe.


Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.


Kwa maana sitasubutu kuongeza kitu kingine, isipokuwa tu kile Kristo alichotimiza kwa njia yangu kusudi watu wa mataifa wapate kumutii Mungu. Alifanya vile kwa njia ya yale aliyoniwezesha kusema na kutenda,


Inafaa mutu yule anayesema vile ajue vema kwamba hakuna tofauti kati ya maneno tunayoandika katika barua zetu wakati tunapokuwa mbali, na yale tutakayofanya wakati tutakapokuwa pamoja nanyi.


Kwa maana, mutu anayekubaliwa si yule anayejisifu mwenyewe, lakini ni yule anayesifiwa na Bwana.


Maneno haya yanaonyesha kwamba tunaanza kujisifu tena sisi wenyewe? Au tunahitaji kuwatolea ninyi barua za ushuhuda au kuziomba kwenu kama wengine?


Sisi hatuanzi tena kujisifu wenyewe mbele yenu, lakini tunawapa ninyi sababu ya kuweza kujivuna kwa ajili yetu. Hivi tena munaweza kupata maneno ya kuwajibu wale wanaojivunia tu hali yao ya inje, lakini si mambo yanayokuwa ndani ya mioyo yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ