Na Krispo, mukubwa wa nyumba ya kuabudia, akamwamini Bwana pamoja na watu wote wa nyumba yake. Nao Wakorinto wengi waliomusikiliza Paulo wakaamini na kubatizwa.
Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo. Mimi ambaye kwa mapenzi ya Mungu, niliitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu. Tunawaandikia kanisa la Mungu linalokuwa Korinto na watu wake wote wanaokuwa katika jimbo lote la Akaya.
Ninawasihi kwamba nitakapofika kwenu, musinisukume kuwa mukali. Kwa maana nina uhakika kwamba nitawatendea vile wale watu wote wanaozania kwamba sisi tunaishi maisha ya kimwili.
Kufuatana na vile ninavyosema ukweli kama vile Kristo, ninaapa kwamba hakuna anayeweza kunizuiza kujivuna juu ya jambo hilo katika jimbo lote la Akaya.
Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.
Ni kwa hiyo ninawaandikia maneno haya nikiwa mbali nanyi, kusudi wakati nitakapokuwa kati yenu nisitende kwa ukali kadiri ya mamlaka Bwana aliyonipa. Kwa maana uwezo ule ni kwa ajili ya kuwajenga katika imani, lakini si wa kubomoa.
Kwa wakati huu ninapokuwa mbali nanyi, ninarudilia kuwaambia waziwazi maneno yale niliyokuwa nimekwisha kuwaambia mbele katika safari yangu ya pili niliyofanya kwenu. Ninawaambia kwamba nitakapokuja kwenu mara tena, sitakosa kuazibu wale waliofanya zambi zamani na wengine wote.
Tunaonyesha kwamba sisi ni watumishi wa Mungu kwa njia ya usafi wa moyo wetu, ya ufahamu, ya uvumilivu, ya wema wetu, ya Roho Mutakatifu, ya upendo wetu wa kweli,