Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 1:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Kama vile Mungu anavyokuwa mwaminifu, hakika mambo tuliyowaambia hayakukuwa ya kusema “Ndiyo” na “Hapana” kwa mara moja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 1:18
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu akasema hivi kwa sauti: “Ndiyo, ninyi munajidai kwamba munanijua na munajua pahali ninapotoka. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini aliyenituma ni mwenye ukweli. Ninyi hamumujui,


Nina maneno mengi ya kusema juu yenu na ya kuwahukumu. Lakini yule aliyenituma ni wa kweli, nami ninajulisha dunia maneno yale niliyosikia kwake.”


Mungu ni mwaminifu katika ahadi zake, yeye aliyewaita ninyi muishi katika ushirika pamoja na Mwana wake Yesu Kristo, Bwana wetu.


Ninamutaja Mungu kuwa mushuhuda wangu, yeye anajua roho yangu! Mimi nilikusudia kutorudia tena Korinto kwa sababu ya kuwasikilia huruma.


Mungu Baba ya Bwana Yesu, anayetukuzwa hata milele, anajua kwamba sisemi uongo.


Basi sisi si kama wengine wengi wanaochuuza neno la Mungu; lakini kwa sababu Mungu ndiye aliyetutuma, sisi tunasema ukweli mbele yake, kama vile watumishi wa Kristo.


Tunaheshimiwa na kuzarauliwa, tunatukanwa na kusifiwa. Tunahesabiwa kama wenye kusema uongo, ingawa sisi tunasema ukweli,


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Laodikia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeitwa ‘Amina’, mushuhuda mwaminifu, mwenye ukweli, na musingi wa viumbe vyote vya Mungu.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Filadelfia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa mutakatifu na mwenye ukweli, anayekuwa na ufunguo wa mufalme Daudi, anayefungua mulango wala hakuna anayeweza kuufunga, anayefunga wala hakuna anayeweza kuufungua.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ