Kulipokucha wabaharia hawakutambua inchi ile lakini wakaona nafasi bahari inapoingia ndani ya inchi kavu na kwenye kivuko. Basi wakakusudia kwenda kukwamisha chombo kule, kama ikiwezekana.
Tumekataa mambo ya kisirisiri na ya haya. Hatuna mwenendo wa udanganyifu wala hatupotowi neno la Mungu. Lakini tunajulisha waziwazi ukweli kusudi tuvute kila mutu kutuaminia katika zamiri yake mbele ya Mungu.
Basi, kwa sababu tunajua kwamba ni lazima kumwogopa Bwana, ndiyo maana tunajitoa kuwavuta watu kwake. Mungu anatujua waziwazi nami ninatumaini kwamba ninyi wenyewe munatujua waziwazi vilevile.