Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 nanyi wenyewe mutatusaidia kwa njia ya maombi. Kwa hivi Mungu atajibu kwa maombi yaliyotolewa na watu wengi kwa ajili yetu na kututendea wema, na watu wengi watamushukuru kwa ajili yetu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 1:11
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”


Basi Petro akabaki akichungwa katika kifungo, lakini kanisa likaendelea kumwombea kwa Mungu pasipo kuchoka.


Kwa maana mambo haya yote yanafika kwa ajili yenu kusudi neema ya Mungu izidishwe kwa watu wengi siku zote, nao wapate kumutolea Mungu shukrani nyingi kwa ajili ya utukufu wake.


Kwa hiyo watawaombea kwa upendo mwingi, kwa ajili ya neema kubwa sana Mungu aliyowajalia.


kwa maana ninajua kwamba kwa ajili ya maombi yenu na kwa musaada wa Roho wa Yesu Kristo nitakombolewa.


Mutuombee sisi vilevile kusudi Mungu atufungulie njia ya kuhubiri neno lake tupate kutangaza ujumbe wa siri juu ya Kristo. Ni kwa ajili ya ujumbe ule mimi niko sasa katika kifungo.


Kwa mwisho wandugu, mutuombee, kusudi neno la Bwana lisambae upesi na kutukuzwa, kama vile inavyokuwa kwenu.


Lakini pamoja na maneno haya, unitayarishie vilevile pahali pa kukaa, maana ninatumaini kwamba Mungu atajibu maombi yenu, na kunijalia nipate kurudishwa tena kwenu.


Muzidi kutuombea. Tuna uhakika kwamba tuko na zamiri safi, kwa maana tunataka kuwa na mwenendo mwema katika mambo yote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ