Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Wakorinto 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo. Mimi ambaye kwa mapenzi ya Mungu, niliitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu. Tunawaandikia kanisa la Mungu linalokuwa Korinto na watu wake wote wanaokuwa katika jimbo lote la Akaya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Wakorinto 1:1
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Paulo akafika Derbe na Listra, ambako kulikuwa mwanafunzi mumoja aliyeitwa Timoteo. Mama yake alikuwa Muyuda, naye alikuwa ameamini lakini baba yake alikuwa Mugriki.


Kwa maana imependeza makanisa ya Makedonia na ya Akaya kukusanya mali kwa kuwasaidia wamasikini wanaokuwa kati ya watu wa Mungu kule Yerusalema.


Timoteo, mutumishi mwenzangu anawasalimia, nao Lukio, Yasoni, na Sosipateri, wanainchi wenzangu wanawasalimia vilevile.


Munisalimie vilevile kanisa linalokusanyika katika nyumba yao. Munisalimie mupendwa wangu Epeneto, anayekuwa mwamini wa kwanza wa Kristo katika jimbo la Azia.


Basi muangalie, kusudi musiwakwaze Wayuda, wala wasiokuwa Wayuda, wala kanisa la Mungu.


Kama Timoteo akifika, mujikaze kumupokea vizuri kati yenu kwa sababu yeye anafanya kazi ya Bwana kama mimi mwenyewe.


Ninyi munajua Stefana na jamaa yake; munafahamu kwamba walikuwa watu wa kwanza walioamini katika inchi ya Akaya, nao wamejitoa kwa kutumikia watu wa Mungu. Hivi ninawasihi sana wandugu zangu,


Ninawapenda ninyi wote katika kuungana na Yesu Kristo.


Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.


Kwa maana Yesu Kristo, Mwana wa Mungu ambaye Silvano, Timoteo na mimi mwenyewe tuliyemuhubiri kwenu hakukuja kusema “Ndiyo” na “Hapana.” Lakini yeye ni “Ndiyo” inayotoka kwa Mungu.


Ninamutaja Mungu kuwa mushuhuda wangu, yeye anajua roho yangu! Mimi nilikusudia kutorudia tena Korinto kwa sababu ya kuwasikilia huruma.


Kufuatana na vile ninavyosema ukweli kama vile Kristo, ninaapa kwamba hakuna anayeweza kunizuiza kujivuna juu ya jambo hilo katika jimbo lote la Akaya.


Kwa maana ninajua nia yenu nzuri ya kusaidia, nami ninajivuna kwa ajili yenu mbele ya watu wa Makedonia, nikisema: “Kanisa la jimbo la Akaya liko tayari kusaidia tangia mwaka jana.” Hivi kwa njia ya bidii yenu mumewavuta wengi kati yao kwa kutoa vilevile.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa wandugu wote wanaokuwa pamoja nami. Ni mimi niliyeitwa kuwa mutume, si kwa kuchaguliwa na watu, wala kwa njia ya mutu, lakini kwa njia ya Yesu Kristo na ya Mungu Baba aliyemufufua. Tunawaandikia ninyi makanisa ya Galatia.


Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo. Mimi niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi watu wa Mungu munaokaa Efeso, munaokuwa waaminifu katika kuungana na Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa Silvano na Timoteo. Tunawaandikia ninyi kanisa la Tesalonika munaoungana na Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo. Tunawatakia neema na amani.


na kumutuma ndugu yetu Timoteo, anayemutumikia Mungu pamoja nasi katika kazi ya kutangaza Habari Njema ya Kristo. Tulimutuma kwenu apate kuwatia nguvu na kuwafariji katika imani yenu,


Barua hii inatoka kwangu, mimi Paulo na kwa Silvano na Timoteo. Tunawaandikia ninyi kanisa la Tesalonika munaoungana na Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tunayemutumainia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, kwa kutangaza ahadi ya uzima tunaokuwa nao katika kuungana na Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Mungu na mutume wa Yesu Kristo. Mimi nimetumwa kwa kuongoza watu waliochaguliwa na Mungu wapate kumwamini na kutambua ukweli unaolingana na dini yetu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo, na kwa ndugu yetu Timoteo. Tunakuandikia wewe Filemono, mupendwa wetu na mwenzetu wa kazi,


Ninapenda kuwajulisha kwamba ndugu yetu Timoteo amekwisha kufunguliwa. Kama akikuja upesi, nitafika kuwaona pamoja naye.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ