na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.
Mara tu Yezebeli alipopata habari kwamba Naboti amekwisha kufa kwa kutupiwa mawe, akamwambia Ahabu: “Simama! Kwenda utwae lile shamba la mizabibu la Naboti wa Yezereheli ambalo alikataa kukuuzishia. Naboti hayuko muzima tena; amekwisha kufa.”
Basi! Yawe anasema hivi: ‘Hakika, nitakuletea maangamizi. Nitakuletea hasa wewe na kuangamiza kila mwanaume wa ukoo wako katika Israeli, akuwe mutumwa au huru.
Lakini ilikuwa imepangwa na Mungu kwamba maangamizi yatendeke kwa Ahazia kwa njia hiyo ya kumutembelea Yoramu; kwa sababu alipofika kule, alitoka pamoja na Yoramu kwenda kupigana na Yehu mwana wa Nimusi ambaye Yawe alimuchagua kwa kuangamiza uzao wa Ahabu.
Na hivi mutabeba lazima ya damu iliyomwangwa katika dunia pasipo kosa, tangia kuuawa kwa Abeli aliyekuwa mukamilifu mpaka kuuawa kwa Zakaria, mwana wa Barakia, muliyemwuia kwenye hekalu katikati ya Pahali Patakatifu na mazabahu.
Wandugu wapendwa, musilipize kisasi ninyi kwa ninyi, lakini mumwachie Mungu wakati wa kutenda kufuatana na kasirani, maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.”
maana yeye anamutumikia Mungu kwa faida yako. Lakini kama ukifanya mabaya, umwogope kwa sababu yeye yuko na uwezo kwa kuazibu. Yeye anamutumikia Mungu wa kuazibu wale wanaofanya mabaya.
Enyi mataifa, mushangilie watu wake, maana yeye analipiza kisasi damu ya watumishi wake, anawalipiza kisasi wapinzani wake, na kuitakasa inchi ya watu wake.
Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!
Hukumu zake ni za kweli na za haki. Amehukumu yule kahaba mukubwa ambaye alikuwa akipotosha dunia kwa vitendo vyake vya uasherati. Mungu amemulipiza kisasi cha damu ya watumishi wake!”
Lakini niko na neno hili juu yako: unamuvumilia yule mwanamuke Yezebeli, anayejiita kuwa nabii wa Mungu. Yeye anawapotosha watumishi wangu akiwafundisha kufanya uasherati na kula nyama za kutambikia sanamu za miungu.