2 Wafalme 9:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
34 na kuingia katika nyumba ya kifalme, na huko akakula na kunywa. Halafu akaamuru: “Muzike mwanamuke yule aliyelaaniwa kwa sababu ni binti ya mufalme.”
Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.
naye Yehu akawaambia: “Mumutupe chini!” Wakamutupa chini na damu yake ikasambaa juu ya ukuta na kwenye farasi. Yehu akapitisha farasi na gari lake juu ya maiti yake
Kwa amri ya mufalme, tangazo hili lilitolewa katika muji mukubwa wa Susani, nao wajumbe wakalitangaza katika majimbo yote. Mufalme na Hamani wakaikaa chini kwa kunywa wakati watu katika muji wa Susani wanafazaika.
“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!